Tuesday, April 9, 2013

MWANAMKE AVULIWA NGUO ZOTE BAADA YA KUINGIA STENDI YA MABASI AKIWA NA SKETI FUPI NYEPESI



 
 Biahara  zote  zilisimama  kwa  muda  katika  stendi  kuu ya mabasi  ya  Bomet  nchini  kenya wikiendi  hii  baada  ya  kundi  kubwa  la  wanaume  kumvamia  mwanamke  mmoja  aliyekuwa  amevaa  kingua  kifupi  na  kisha  kumvua  huku  wengine  wakimchezea  nyeti  zake.....
Mwanamke  huyo ambaye inadaiwa  alienda  katika  stendi  hiyo  kufanya  booking  ya  basi,alikutwa  na  kisanga  hicho  baada  ya  kuvamiwa  na  kundi  kubwa  la  wapiga  debe  na  vibaka  ambao  walianza  kwa  kumzomea  na  kumrushia  makopo  ya  maji......

Kwa  mujibu  wa  shuhuda  wa  tukio  hilo,sakata  hilo  lilichukua  takribani  dakika  15  za  kumzomea  na  kumtukana  wakiwa  wamemzunguka  kabla  ya  kumvua  nguo  zake.....

"Walimzomea  na  kumtukana  vibaya  huku  wakiwa  wamemzingira.Juhudi za  wanawake  wasamaria  wema  kumuokoa  zilikwama  kwa  kuwa  kundi  lilikuwa  kubwa  na  wao  walikuwa  wanaogopa  kufanyiwa  hivyo"...Alisema  shuhuda  huyo

Mbali  na  shuhuda  huyo,Bwana  Sang  naye  analielezea  tukio  hilo  kwa  kudai  kuwa  ile  sketi  ilikuwa  ni  zaidi  ya  fupi  na  pia  ilikuwa nyepesi  na  ndani  ndani  hakuwa  na  kitu, hali  iliyosababisha  wapiga  debe  hao  wamvae  na  kumvua.....

Bwana  Sang  anadai  kuwa  kesi  nyingi  za  ubakaji  zimekuwa  zikisababishwa  na  wanawake  wenyewe  kutokana  na  mavazi  yao  wanayoyavaa....

Baada  ya  tukio  hilo  kupamba  moto, polisi  walifika  japo  walichelewa  na  hatimaye  kufanikiwa  kumwokea  mrembo  huo  mikononi  mwa  vibaka  hao....

Kutokana  na  tukio  hilo,shirika  la  maendeleo  ya  wanawake  limelaani  vibaya  tukio  hilo  na  kuahidi  kuchukua  hatua  kali  zaidi  endapo  udhalilishaji  huo  utaendelea  na  kufumbiwa  macho....

No comments:

Post a Comment