Friday, May 31, 2013

MABADILIKO KUHUSU MAZISHI YA NGWEA



Habari kutoka kwa wanakamati wa mipango ya mazishi ya marehem Albert Mangwea zinasema kuwa mwili wa marehem Ngwea utafika Dar siku ya jumapili saa nane mchana na sio jumamosi kama ilivyoarifiwa hapo awali…


Mwili huo utaagwa siku ya jumatatu saa mbili mpaka saa sita machana ambapo safari itaanza kuelekea Morogoro kwa ajili ya mazishi

KIJANA ANUSURIKA KUFA BAADA YA VIBAKA KUMCHOMA MOTO HUKO MKOANI LINDI



Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ismai Mayoba(31) anayefanya kazi Bar ya Mangrove,Mkazi wa Manispaa ya Lindi amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kundi la Vijana waliotaka kumpora na hatimae kumchoma moto. 

Kwa sasa kijana huyo amelazwa katika Hospital ya Sokoine Mjini humo.

Kufuatia tukio hilo,Jeshi la Polisi wilayani Lindi limefanikiwa kumkamata mtu  mmoja kati ya watuhumiwa saba waliohusika na tukio hilo lilitokea katika eneo la Mtaa wa Congo.


Akithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kukamatwa kwa mtuhumiwa,Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi,Renatha Mzinga alimtaja ndugu Ally Manially(22)mkazi wa mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa na Jeshi hilo na atafikishwa mahakamani leo kujibu shitaka la kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia ya Udanganyifu ikiwa pamoja na kumchoma mwenzie Moto huku akijua ni kosa kisheria.

Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea kutafuta watuhumiwa wengine 6 waliohusika na tukio hilo

ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU NDOA ZA JINSIA MOJA.....UKINASWA IMEKULA KWAKO ( MIAKA 30 JELA )




Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imetunga sheria ya kupiga marufuku ndoa za watu wa jinsia moja.Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Bwana Abubakar Khamis Bakar, aliyasema hayo kwenye Kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi, Saleh Nassor Juma kutoka Chama cha Wananchi (CUF).

Katika swali lake, Bw. Saleh Nassor Juma alitaka kujua ni lini Serikali ya Zanzibar itatunga sheria ya kukataza ndoa hizo na kuweka adhabu kali kwa watu ambao watabainika kufanya vitendo hivyo vichafu. 


Waziri Abubakar amesema, ndoa za watu wa jinsia moja ni kinyume na utamaduni wa Zanzibar na kwamba sheria hiyo imeweka adhabu ya kifungo cha miaka saba kwa wale wote watakaopatikana na hatia hiyo.

Pia alisema kama ninavyomnukuu: "Sheria hii inahusu makosa mengi yakiwemo ya ubakaji, zinaa, usagaji na umalaya ambayo yote yana adhabu ya kifungo cha maisha au miaka isiyopungua 30 gerezani," mwisho wa kunukuu.

HUYU NDO MSHIRIKI WA BBA KUTOKA ZIMBABWE ALIYE CHEZA MKANDA WA NGONO.....WANANCHI WAMEJIPANGA KUMNG'OA



Mshiriki wa shindano la Big Brother Africa Chase kutoka nchini Zimbabwe Nare Pokello amejikuta katika kashfa kubwa baada ya mkanda wake wa ngono kuvuja siku chache tu baada ya yeye kuingia ndani ya jumba la BBA.

 kashfa hiyo ambayo sasa ndio habari ya mjini imezagaa  katika  kurasa kadhaa za Facebook huku mashabiki wengi kutoka nchini kwake wakisistiza watu wampigie kura ya kumng'oa  Pokello nje ya jumba hilo  . 

Mashabiki hao wametengeneza ukurasa hivi karibuni, ambao unashinikiza watu wapige kura za kumng'oa Pokello katika jumba hilo la BBA, Ukurasa huo ulioundwa wiki hii mpaka sasa tayari una zaidi ya wafuasi zaidi ya 4 000.
Katika video hiyo ya ngono, Pokello na mpenzi wake "Desmond Chideme " maarufu kama Stunner wanaonekana wakifanya ngono bila kutumia kinga.

Video hiyo ambayo ilirekodiwa kwa kutumia simu ya iphone na kubadilishwa kwenda kwenye fomati ya avi ilivuja baada ya boyfriend wa pokello kuitoa video hiyo na kumpa rafiki yake wa karibu huku akijisifu.

Katika video hiyo, Stunner anaonekana akizungumza mbele ya kioo cha kamera huku Pokello akiwa anatabasamu. 


video mwishoni inamwonyesha, Pokello akiwa ana ananyonya uume wa Stunner huku Stunner akisema 'wewe msichana ni kituko'.

Chanzo kimoja kilisema Pokello alivujisha video yake mwenyewe na kudai kama siyo yeye aliyevujisha ni Kwa nini alikubali kufanya hivyo kama hawakuwa na nia ya watu kuiona?

Thursday, May 30, 2013

K' LYNE AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA REGINALD MENGI



Kumekuwepo na Minong'ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili. 

Hongera Mmiliki  wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali  Jackline Ntuyabaliwe(K'lyne)  ....

Hiyo ndo Tweet ya K'lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI

MBINU ZA KIMAHABA ALIZOZITUMIA KARRUECHE TRAN KUUTEKA TENA MOYO WA CHRIS BROWN




Kwa kawaida mapenzi hutawaliwa na hisia za kimahaba alizonazo mtu kwa mwenziwe ama mtu anaetamani kuwa nae kama boyfriend/girlfriend wake ama mke/wake. Lakini hakukosea aliyesema mapenzi ni kama mmea unaweza kutunzwa na kustawi na ukiachwa bila matunzo unaweza kunyauka. 


Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa mrembo Karrueche Tran aliyetoswa vibaya na Chris Brown lakini kwa kuweka mikakati ya dhati na kuumwagilizia vyema mmea wa penzi kati yake na na Chris hata wakati akiwa hana muda nae na anahang out na Rihanna kumemsaidia kurudisha kwa kasi na nguvu mpya penzi alilopoteza.
 
Moja kati ya mikakati ya kimahaba aliyoitumia Karrueche huku moyoni mwake akiuamini msemo wa ‘mvumilivu hula mbivu’, ni kujiweka karibu na Chris kama rafiki hata wakati akiwa bado yuko na Rihanna na hakuonesha chuki ya wazi kwake japokuwa alikuwa anaumia sana. 


Mkakati mwingine ni kuhakikisha anaonesha moyo wa upendo wa dhati na nia ya kuwa na Chris Brown kwa kuwa alijua kabisa kuwa mwisho wa siku ataangalia zaidi anakooneshwa kupendwa na kuvumiliwa, akijua mwisho wa siku akiumizwa na kulizwa huko aliko atahitaji kufutwa machozi na kutulizwa, na Karrueche atakuwa karibu zaidi, na kweli ndicho kilichotokea.



Chanzo cha karibu na KT kimesema, “Karrueche hakuwahi kuacha kumpenda Chris, hakuwa kulazimisha kitu chochote kwake kwa upande wa mahusiano, na hakuwahi kulazimisha kupewa kitu mkononi au kuomba chochote kwake.”



Mkakati huo pia ulimuongezea alama za ushindi kwa jamaa, lakini pia alijua kabisa ya Rihanna yatapita tena, kwa imani yamepita kweli. “Alijua alikuwa bado anafanya vyote na Rihanna na alitegemea hilo na muda wote alikuwa rafiki kwa Chris Breezy hata wakati akiwa na Rihanna.” Kiliendelea kufunguka chanzo hicho.



Kwa sasa KT amehamia nyumbani kwa Chris na ripoti zinasema ni takribani nusu mwezi hivi na wanaishi kama mke na mume.

AIBU YA BIG BROTHER: VIDEO ZA MAPENZI ZAANZA KUONEKANA KATIKA NYUMBA ANAYOIONGOZA FEZA KESSY WA TANZANIA



Ikiwa ni usiku wa pili (usiku wa kuamkia leo)katika reality show ndani ya jumba la Big Brother Africa mwaka huu lilipewa jina la ‘The chace’ mambo mengi mapya yameanza kuonekana kwa washiriki ambao wameanza kufahamiana.
 
Katika hali ambayo mara nyingi haikwepeki hasa wanapokutana wanawake warembo na wanaume watanashati, scene za mapenzi zimeanza kuonekana katika Diamond house inayoongozwa na mtanzania Fezza Kessy (Head of house) ....

‘Bolt’ , mshiriki kutoka Sierra Leone na Betty ambae ni mshiriki kutoka Ethiopia walipata nafasi ya kufahamiana zaidi na kuvuka mstari wa urafiki wa kawaida wakati washiriki wengine wakiwa wamelala  ndani ya jumba la Kessy
Betty na Bolt..

Betty ambae yuko nominated pasipo yeye kufahamu, sasa yeye na Bolt ndio waliothibitishwa kuwa couple ya kwanza, japo hatima ya mahusiano yao huenda ikawa hatarini kwa kuwa jumapili hii kura za watazamaji zitaamua hatima ya Betty kuendelea kuwa katika jumba hilo au kurudi Ethiopia. 

"SITAKI KUSIKIA NYIMBO ZA NGWEA ZIKIPIGWA CLOUDS FM..WAO NDO WALIOMFANYA AANZE KUVUTA BANGI ILI KUONDOA MAWAZO"...P FUNK




Muda mfupi uliopita djchoka amepokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anayejulikana kwa jina la P Fuck Majani na kumuuomba aipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi.

Tuesday, May 28, 2013

CHANZO CHA KIFO CHA MSANII ALBERT MANGWEA



Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.

Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear  na   M to the P  ambaye walikuwa room moja walitakiwa kurudi Tanzania leo  wakitokea  Afrika kusini..

Walipowapitia,  waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya...
 
Mpaka sasa M to the P yupo hoi  katika  hospitali ya St. Hellen  huku  msanii Ngwair  akiwa  tayari  amekwishaaga  dunia.....

Tunaendelea  kufuatilia  undani wa  tukio  hili

R.I.P NGWAIR 

Mke wa Mshikaji Wangu Aniduwaza!



Jana nimeduwazwa sana baada ya mke wa rafiki yangu kunitamkia wazi kuwa ananipenda na anataka kutoka na mimi.
Tangu nifahamiane naye miaka takribani mitano sasa tumekuwa tukiheshimiana naye sana kama mashemeji. mwaka huu akaniambia kuwa mumewe ameanza kubadilika kwa kuzidisha ulevi, kuchelewa kurudi nyumbani na wakati mwingine kulala nje na pia alizifuma meseji za mapenzi kwenye simu ya mumewe kutoka kwa mtu aliyemsave kwa jina la kiume, hivyo nimsaidie kumshauri ili abadilke ila akanionya nisimwambie kama ni yeye ndiye kaniambia.

Nilimtia moyo kuhusu hali hiyo na kumwomba awe mvumilivu na asichoke kuongea na mumewe kuhusu hali hiyo ili abadilike. Binafsi nilipata wakati mgumu wa namna gani nitamshauri jamaa bila kumtajia makosa yake na wapi nimeyapata hivyo nikashindwa hiyo kazi.
 

Mke wa jamaa akaanza kunipigia simu usiku kulalamika kila mumewe anapochelewa kurudi na wakati mwingine akinipigia alfajiri kuniambia kuwa mumewe hajarudi hadi muda huo. Niliendelea kumtia moyo ingawa mambo hayo yalikuwa ni ya kweli.
 

Cha ajabu kuanzia wiki jana amekuwa akinitumia meseji za mapenzi, nikajua ni hizi meseji ambazo watu hutumiana hivyo sikujali sana hadi pale aliponiandikia akiniambia kuwa yuko serious anataka kutoka na mimi. Sikuamini nikampigia simu kusikia sauti yake kama ni yeye kweli, ndipo aliponithibitishia kuwa yuko serious na atatunza siri na kunitunzia heshima yangu kwa jamaa kwani tayari moyo wake umeangukia kwangu.
 

Sikuweza kumjibu kitu kwa namna nilivyopatwa na mshangao. hadi sasa anaendelea kunibembeleza na kunipa mbinu nyingi za kutimiza lengo lake bila kujulikana na watu.
 

Binafsi sina lengo la kumsaliti mshikaji wangu ila nimelileta kwenu ili mnishauri nimjibu vipi huyu mwanamke ili heshima yangu kwa familia hii iendelee kuwapo na pia kusitokee chuki yoyote kutokana na kadhia hii itakayopelekea urafiki wangu na familia hii kuyumba au kupotea.

AIBU: KIJANA ANASWA AKIUZA UUJME WA MTU....POLISI WATIA MBARONI



Jeshi la polisi nchini malawi wanamshikilia kijana mmoja baada ya kumkuta akiuza sehemu ya siri ya mwanaume.

Kijana huyo mwenye miaka 24 alikamatwa baada ya wananchi kutoa ripoti kituo cha polisi kuwa kunamzee kalala relini huku akiwa anatokwa damu nyingi 
 Polisi walifika eneo la tukio na kumkuta mzee huyo akiwa hoi na kuamua kumkimbiza hosipitali.

Baada ya kufikishwa hosipitali, madaktari  gundua kuwa mzee huyo alikuwa amejeruhiwa kwa kukatwa sehemu zake za siri...

Madaktari hao walilipoti kwa maofisa hao wa polisi na ndipo msako mkali ulipo pita katika wilaya ya Lakeshore mjini Salima na polisi hao kufanikiwa kumtia mbaroni kijana huyo baada ya kumkuta  akiwa katika gesti bubu akijaribu kuuza uume huo kwa dola za kimarekani 360.
  Mtuhumiwa Samuel Banda

Polisi walisema mtuhumiwa Samuel Banda alikamatwa na kiungo hicho ambacho alikuwa amekifunga katika karatasi nyeupe.

Mtuhumiwa alikiri kuwa huwa anauza viungo mbalimbali vya binadamu kwa wafanya biashara maarufu nchini humo ambao wanaamini wakivipata viungo hivyo huwasaidia katika biashara zao na huwaongezea utajiri.

AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA WA MIAKA 7


MKAZI wa kijiji cha Turiani, Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Athuman Rashid (25) amehukumiwa kutumikia kifungo cha maisha jela na adhabu ya kuchapwa viboko sita baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka saba. 
Hukumu hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Korogwe, Arnold Kirekiano.

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyosomwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Janson Zakaria alidai Athuman alitenda kosa hilo Juni 21 mwaka jana, saa 11.00 jioni katika kijiji cha Turiani wilayani hapo. 
 
Hati hiyo ya mashitaka inadai Athuman alimuita mtoto huyo ambaye alikuwa akiishi na bibi yake kijijini hapo kwa lengo la kumtuma dukani ndipo alipomtendea unyama huo. 
 
“Alipokuwa akifanyiwa tendo hilo mtoto huyo alipiga kelele na baadhi ya majirani kujitokeza kufika eneo hilo huku, mtoto huyo akilalamika kwa maumivu sehemu ya siri na akimtaja mtuhumiwa,” alidai Zakaria. 
 
Kabla ya Hakimu Kirekiano kutoa hukumu alimtaka mshitakiwa kama ana chochote cha kujitetea aeleze mahakamani; naye akasema hana cha kujitetea, Mahakama iamue. 
 
Hakimu alisema kifungo hicho cha maisha jela na viboko sita, iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

DIVA WA CLOUDS FM AMPA SUPPORT "MKE MWENZA WA KENYA " ANAYEIWAKILISHA NCHI HIYO KWENYE BIG BROTHER AFRICA


juzi (May 26) ndio ulifanyika ufunguzi rasmi wa shindano kubwa Africa la Big Brother ambalo mwaka huu limepewa jina la “The Chase”, na tayari washiriki wa nchi zote ikiwemo Tanzania wamekwisha fahamika.

Huddah Monroe a.k.a The boss lady ambaye ni model mwaka huu ndio amebeba imani za wakenya za kurudi na kitita cha $300,000 zinazoshindaniwa katika msimu wa 8 wa shindano la Big Brother “The Chase” baada ya kuchaguliwa kuiwakilisha nchi hiyo ya jirani. 
 
Siku chache zilizopita jina la Huddah limeonekana kupata umaarufu zaidi Tanzania hasa kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, baada ya binti huyo mwenye historia ya matukio mengi ya utata huko Kenya (pamoja na kujihusisha na upigaji wa picha za utupu) kujikuta anaingia katika ugomvi wa maneno na mtangazaji maarufu hapa Tanzania Loveness Love a.k.a Diva kutokana na kinachoaminika kuwa sababu ni Prezzo. 
 
Diva a.k.a mimi Kupitia akaunti yake ya twitter, juzi (May 26) aliandika tweet inayoonesha kuweka kando tofauti alizokuwa nazo na Huddah na kuahidi kumsupport kwa kutokumwandikia “shit” kama njia ya kumuunga mkono “wifi” katika BBA.

Diva amekuwa akidai kuwa na mahusiano ya kimapenzi na rapper kutoka Kenya CMB Prezzo, kitendo kilichopokelewa tofauti na mrembo Huddah ambaye pia kulikuwa na tetesi aliwahi kudate na “Liq Her” hit maker, Rapcellency, Prezzo.

Monday, May 27, 2013

JACK WOLPER ALIA NA MATAPELI YANAYOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA JINA LAKE KUOMBA HELA WATU



Katika kile kinachoonekana ni mwendelezo wa matapeli wa mjini kutumia majina ya waigizaji maarufu nchini kutapeli watu kwa njia ya mtandao, dhahama hii sasa imemkuta mwanadada Jacqueline wolper baada ya watu wanaoaminika kuwa ni matapeli kutumia jina lake kujipatia fedha na vitu vingine kiudanganyifu.

Akizungumza kwa simu na tovuti ya bongomovies, mwanadada Jacqueline wolper  alisema matapeli hawa sasa wameamua kutumia mtandao wa instagram na mtandao mwingine wa kijamii uitwao badoo kwa jina la “wolper gambe25” katika kutapeli watu kwa kuwaomba hela au michango mbalimbali kupitia account hizo feki

“Leo nilikuwa naenda saluni, baada ya kufika tuu, yule dada wa saluni akaanza kunilalamikia kuwa mbona sijaenda kuchukua viatu nilivyomuagiza pamoja na hela? 

  
Nikawa sijui cha kumwambia maana sikumuagiza viatu na wala sijampigia simu kumwambia anitumie hela, ndipo aliponionesha huo ujumbe kwenye simu yake na ndio nikagundua hizo account feki za hao watu wanaoutumia jina langu kutapeli watu” Alisema Jack.

“Mimi sipo facebook na wala sitarajii kujiunga, nawaomba sana mashabiki wangu wajue hilo. Natumia mtandao wa instagram kwa jina la wolpergambe au jacklinewolperjacklinewolper.”
 Alisisitza Wolper

Pia alisema kuwa amegundua leo kuna mtu mwingine anayetumia jina lake kuomba watu wamchangie kuhusu kampeni inayoitwa“Zinduka” na amewataka sana mashabiki wake wasije wakafanya hivyo kwani mtu huyo ni mwizi na analengo la kumchafulia jina lake.

HII NI NEEMA KWA WALIOFELI KIDATO CHA NNE....UFAULU WAONGEZEKA, MATOKEO NI MUDA WOWOTE


Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.

Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.

Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.

Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.

Msemaji wa Necta, John Nchimbi alisema upangaji wa matokeo hayo ulikuwa bado unaendelea. “Ninachojua kwa sasa ni kuwa mchakato unaendelea na matokeo yatatangazwa mapema tu ili watoto waweze kujiunga na shule mapema,” alisema Nchimbi.

Pia alisema usahihishaji wa mitihani ya kidato cha sita umekamilika.

Matokeo ya awali

Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.

Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,909 sawa na asilimia 65.5 walipata sifuri, hesabu ambayo imebadilika katika matokeo mapya ambayo yanaonyesha kuwa sasa waliopata daraja hilo ni 158,100 ambayo ni asilimia 43.

Hata hivyo, habari kutoka Necta zinasema kuwa licha ya kuwezesha kuongezeka kwa waliofaulu, matumizi ya kanuni mpya ya kukokotoa matokeo hayo yalisababisha zaidi ya wanafunzi 2,500 kushuka ufaulu ikilinganishwa na awali.

Maofisa mbalimbali wa Necta pamoja na wale wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na taasisi zake, walikutana mwishoni mwa wiki iliyopita kukubaliana masuala mbalimbali juu ya matokeo hayo pamoja na suala la matokeo ya wanafunzi hao 2,500 kabla ya kutangazwa wiki hii.

“Baada ya wajumbe kujadili suala lile, busara ilibidi itumike kwa hiyo hakuna mwanafunzi ambaye alama yake itashuka, kwa kawaida isingewezekana mtoto ambaye matokeo yalitoka akiwa amefaulu leo umwambie ameshuka,” kilieleza chanzo chetu.
Matokeo ya awali ndiyo chimbuko la kupitiwa upya baada ya wadau kuyalalamikia na kumlazimisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuunda tume ya kuyachunguza Februari 23, mwaka huu.
Kabla ya tume hiyo kuhitimisha shughuli zake, ilitoa taarifa ya awali ambayo ilipendekeza kufutwa kwa matokeo hayo kwa maelezo kwamba Necta ilitumia kanuni mpya ya kukokotoa matokeo bila kushauriana na wadau.
Serikali ilitoa taarifa bungeni kwamba imeamua kufuta matokeo ya 2012 na kuamuru yapangwe upya kwa kufuata madaraja yaliyotumika mwaka 2011.

RIHANNA IMEKULA KWAKE..!!!!! ...KARRUECHE TRANS SASA AHAMIMIA NYUMBANI KWA CHRIS BROWN




Siku zote mwenye kiu iliyopitiliza akipewa maji ya kunywa hutamani atumie jagi zaidi ya kikombe anachowekewa maji, ndivyo ilivyomtokea mrembo Karrueche Tran aliyetoswa mwaka jana na Chris Brown aliyemchagua Rihanna dhidi yake wakati mrembo huyo akiwa na moyo uliojaa mapenzi na maumivu ya kulikosa penzi la ‘turn up the music singer’..
Sasa alipopewa nafasi tena ameamua kuitumia vyema na katika kupunguza zaidi umbali ameamua kuhamia kabisa nyumbani kwa mwimbaji huyo. 


Kwa mujibu wa TMZ Chris na Karrueche wamekua wakiishi pamoja nyumbani kwa muimbaji huyo Los Angeles tangu walipoonekana pamoja kwenye sherehe ya kuzaliwa Chris Brown alipotimiza miaka 24. 
Ripoti zinasema mrembo huyo amehamishia nguo zake na vitu vyake takribani vyote kutoka kwake na kuvipeleka nyumbani kwa Chris Brown lengo ni kuwa karibu zaidi na mwimbaji huyo. 

Rafiki wa karibu wa KT ameuambia mtandao wa Hollywoodlife kuwa karrueche anajaribu kuweka commitment katika mahusiano yake na Chris ambayo mwimbaji huyo hawezi kuitunza lakini ameamua kujiweka kwenye mstari huo kwa ajili ya mahusiano yao. 

Chanzo hicho kiliongeza kuwa Karrueche anampenda Chris kwa sababu wanaendana na anapenda upande mwema wa Chris Brown. 

Inawezekana Karrueche hamhofii tena Rihanna kwa kuwa mwaka jana alilazimika kuisomba mizigo yake kutoka kwenye nyumba ya mwimbaji huyo baada ya kumwagwa na himaya yake kuchukuliwa na RiRi bila sababu za msingi isipokuwa Chris kuamua tu kumrudisha RiRi. 


Kwa sasa Chris na Rihanna hawako pamoja tena na Karrueche anaonekana kukaba nafasi yake vizuri. Swali, je hii pembe tatu ya mapenzi yaliyojaa drama itaishia hapo au baadae itambidi KT aondoe tena mizigo yake kumpisha Rihanna?

PENZI LA WASTARA LAGOMBANIWA.....



TAKRIBAN  wiki moja baada ya kumaliza eda tangu alipofariki mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari 2, mwaka huu, staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma anagombewa na midume ikitaka kumuoa.


Akizungumza na mwandishi wetu  akiwa nchini Oman, Wastara alifunguka kuwa tangu amalize eda yake hiyo amekuwa akipata usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume mitandaoni na wanaomtamkia mwenyewe.

“Jamani mpaka nahisi kuchanganyikiwa kabisa, wanaume zaidi ya mia tano hata sijui walipotokea wanataka kunioa, hadi nahisi majanga,” alisema Wastara.

Wastara alisema kuwa wanaume hao wamekuwa wakihangaika bure kwa sababu kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa kwani anapotembea bado anasikia harufu ya mumewe Sajuki.
 
“Bado harufu ya Sajuki ipo mwilini mwangu, wanaume wanaonitolea macho mtoto wa mwenzao wanakosea sana, sifikirii kabisa suala hilo kwa sasa,” alisema Wastara mwenye mtoto mdogo aliyezaa na Sajuki.

LWAKATARE AKWAMA TENA KUPATA DHAMANA, KESI YA JAYDEE YARUSHWA MPAKA JUNE 13.

LWAKATARE AKWAMA TENA KUPATA DHAMANA, KESI YA JAYDEE YARUSHWA MPAKA JUNE 13.

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Wilfred Lwakatare na mwenziye Ludovick Joseph wamekwama tena leo Jumatatu, Mei 27 kupata dhamana baada ya Hakimu Mkazi katika Mahakama ya Kisutu, Sundi Fimbo kueleza kuwa Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Aloyce Katemana, bado yupo likizo tangu wiki tatu zilizopita.
  
Watuhumiwa wanakabiliwa na shitaka la kupanga njama za kumnywesha sumu Mhariri wa Gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky.

Lady Jay Dee akiwa na mumewe Gardner Habash wakisuburi kesi kutajwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kindondoni leo asubuhi saa tatu. 
------------------
Mwanamuziki Judith Wambura-Habash --Lady Jay Dee-- alifika katika mahakama ya Kinondoni leo kama ilivyotakiwa kwa mashitaka aliyofunguliwa hapo. Baadaye amefahamisha kuwa ameambiwa ardui tarehe 13 Juni 2013.
Kesi imetajwa tena tar 13 June 2013. Saa 5 asub.

Wednesday, May 22, 2013

KAKA NA DADA WANASWA WAKIVUNJA AMRI YA SITA KATIKA MAPANGO YA UFUKWE WA COCO





UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya mapenzi   kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi

Imefahamika kwamba vijana  hao, kaka na dada   wamenaswa ‘wakingonoka  katika mapango yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.


Tukio zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska usiku na mchana.

Risasi  lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
 
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.



Haikufahamika mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
 
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.

Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera zetu.
Ni kama vile hawakuwa na makubaliano na kile walichokuwa wakienda kukifanya.
 
Mara kadhaa dada huyo alionekana kumkwepa kaka yake na alikuwa akijiondoa karibu yake pale alipomlazimisha kutaka kumfanyia kitu kisichokuwa cha kawaida.



Kamera za Risasi ziliwafuatilia wawili hao kwa kuwa walionekana kuwa na kitu ‘spesho’. 

 Mpaka wanazama katika mapango yaliyopo kando ya ufukwe huo wa Coco, kamera zilikuwa zikiendelea kuwachukua hadi walipozama ndani kabisa ya mapango hayo. 
 

Walipozama ndani ya mapango hayo, ghafla walitokea askari ambao nao walikuwa wakifuatilia nyendo za wawili hao.
 

Askari hao wa Kituo cha Oysterbay, wakiongozwa na kamanda wa oparesheni maalumu katika Wilaya ya Kinondoni, Kamanda Swai walifuatilia kwa umakini tukio hilo.
 

Wakiwa chini ya mapango, kaka na dada waliondoa vinguo vilivyokuwa maungoni mwao na kuanza kuduu kama vile walikuwa katika ufukwe unaoruhusiwa kufanya vitendo hivyo.
 
Kabla askari hawajawavamia, waliwashuhudia wawili hao wakiwa katika kilele cha sterehe yao huku dada mtu akionesha kutoa ushirikiano kwa shingo upande.


Ghafla, askari waliwavamia na kuwatibulia starehe yao kisha kuwatia mbaroni.
 

Baada ya kuona kuwa wamevamiwa na askari, kaka mtu alichomoka na kutafuta silaha ili kuweza kujihami na wavamizi wake bila ya kujua kama ni askari.
 

Katika hilo nusura zipigwe kati ya askari na kaka huyo ambaye alikuwa akitaka kupigana na watu asiowajua kwa kuwa walikuwa wametinga mavazi ya kiraia.
 

Hata hivyo, alitulizwa na kutakiwa kuvaa pensi yake ili aweze kutoa maelezo kwa kina. 
 

Wakati yote yakiendelea, dada mtu alikuwa amepigwa na butwaa na kutojua cha kufanya hadi aliporushiwa kitenge chake kilichokuwa pembeni ili ajisitiri mwili wake. 

Katika mahojiano ya awali yaliyoongozwa na Kamanda Swai, ilibainika kwamba wawili hao ni ndugu wa damu yaani kaka na dada.  

Maelezo hayo yanasema kuwa dada mtu alitoka mkoani na alikuja kutembea jijini Dar es Salaam, ndipo kaka yake alipomtaka watoke kwenda kumuonesha vivutio vya jiji hilo. 

“Nina miaka 19, nimetokea Iringa kuja Dar kutembelea familia lakini kaka akanileta huku na kunifanyia vile, siyo kama tulikuwa tumekubaliana,” alisema dada huyo kwa aibu.

Kaka mtu alikiri kile kilichosemwa na dada yake na kushindwa kujitetea kwa kuwa kila kitu kilikuwa hadharani. 


Wawili hao walichukuliwa na kupelekwa katika Kituo cha Oysterbay kwa ajili ya kufunguliwa kesi ya uzembe na uzururaji na kusekwa rumande kabla ya kufikishwa mahakamani.

KUNDI LA CAMP MULLA LAZIDI KUPASUKA....



Hivi karibuni tuliandika habari kuhusu kundi linaloundwa na vijana wanne wenye vipaji kutoka Kenya linalofahamika kama Camp Mulla kumpoteza member mmoja ambaye ndio aliyekuwa msichana pekee katika kundi aitwaye Miss Karun.


Mwanzo ulianza kama uvumi kuwa Miss Karun amepigwa chini na kundi hilo na nafasi yake kuchukuliwa na msichana mwingine aitwaye Tiri, lakini habari mpya habari zilizothibitishwa Kupitia mtandao wa kituo kikubwa Africa Kusini Channel O, zinasema Miss Karun ameamua kujiondoa kwenye kundi kwaajili ya maandalizi ya kujiunga na chuo. 
  

Miss Karun anategemewa kwenda masomoni nchini Marekani mwezi August mwaka huu, lakini ataendelea kufanya muziki kama solo.

camp m

Kama vile haitoshi, kwa mujibu wa mtandao huo member mwingine aitwaye Thee Mc Africa zamani alifahamika kama Taio Tripper naye amejitoa katika kundi hilo na ataendelea kufanya muziki kama solo. 
  

Kundi hilo lilianzishwa mwaka 2009 likiwa na members wanne, Kwa sasa limebaki na members wawili wa mwanzo pamoja na msanii mpya wa kike aitwaye Tiri.

VURUGU ZA MTWARA ZASABABISHA BUNGE LIAHIRISHWE....




Spika wa bunge , Anne Makinda ameahirisha Bunge kutokana na hali ya Mtwara na ameiagiza serikali kuwa kesho wawasilishe taarifa bungeni kuhusiana na hali hiyo.

Makinda ameitisha kamati ya uongozi ili kuona kama wanaweza kutuma kamati ya Bunge kesho kwenda huko.

UKICHECHE WAMFANYA MR. NICE AZOMEWE NCHINI KENYA




Mtandao wa ghafla kutoka Kenya umeripoti kuwa, msanii Mr Nice, amejikuta akizomewa na umati wa watu waliokuwa katika Club moja inayoitwa I club, ambapo wachekeshaji Fred Omondi na Mc Antonio hufanya show zao pale kila siku za jumapili.

Inasemekana Mr Nice alikua ameenda pale kwa ajili ya kula good time tu, na kufurahisha nafsi yake, lakini matokeo yake hayakuwa kama alivyotarajia....

Aibu  ilianza pale mchekeshaji Mc Antonio alipomuona Mr Nice katikati ya watu, na kwakuwa ni mtu maarufu, Mc akamuambia awapungie mikono watu waliokuwepo pale...


Mr Nice hakufanya hivyo wala kusimama akidai kuwa yeye ni msanii ambae amesainiwa na mtu mwingine na Mc huyo hawezi kumlipa yeye, na akipanda jukwaani hapo atashitakiwa na magement yake.
 
 " Hamnilipi ninyi... nikipanda hapa kwenye jukwaa, nitashtakiwa mimi"..Mr.Nice

Baada ya kusema maneno hayo mashabiki walianza kumzomea huku wakipiga kelele wakisema Mac "Muga" wimbo  wa Ally Kiba, ambao unasemekana kuwa unamdiss yeye. na dj hakuwa na hiyana aliupiga wimbo huo maana mashabiki waliutaka.

Djfetty

"WASANII WANAOVAA VIMINI KWENYE FILAMU HUWA WANAJIUZA"....MWAKIFAMBA




RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifwamba amesema wasanii wanaovaa mavazi yasiyo na staha ikiwemo vimini kwenye sinema wanajiuza.

Mwakifwamba aliyasema hayo katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, akiwa ameongozana na msanii Riyama Ally.
 

Kauli hiyo ya Mwakifwamba imekuja siku chache baada ya sakata la uvaaji vimini na udhalilishaji wanawake na wototo kwenye filamu kuzungumziwa bungeni, Dodoma.

“Hili suala nimeshalikemea kwa muda mrefu sana... naamini kama ni watu wa kuelewa watakuwa wameelewa na wale ambao wanaendelea na hayo mambo maana yake ujue wana mambo yao.


“Siyo wote wanaoingia kwenye filamu ni wasanii wa kweli, wengine wanatumia tasnia hii kutafuta mabwana ndiyo maana wanavaa mavazi ya ajabu ili waonekane, jambo ambalo tunalikemea kila wakati

"Sikatai wakati mwingine kuna ‘scene’ zitahitaji uhusika fulani kama uchangudoa lakini utakuta msanii anatakiwa kuvaa uhusika wa ofisini, yeye anavaa vinguo vya hovyo, maana yake ni nini kama si kutafuta soko?” alisema Mwakifwamba na kuongeza:
 

“Imefika wakati wasanii wanatakiwa wabadilike kwani hali ilipofikia siyo pazuri. Bado msanii anaweza kuonekana ana kiwango kizuri bila kuvaa nguo zinazomdhalilisha na kumtafsiri vibaya mbele ya jamii.”
 

Akasema: “Sasa nasema hivi, yeyote atakayekiuka utaratibu tuliokubaliana tutamchukulia hatua. Hatutamfumbia macho. Tunahitaji kuwa na tasnia yenye heshima.”
 

RIYAMA SASA
Mkali wa kucheza na hisia, Riyama naye alitoa maoni yake kuhusu mavazi na mwenendo mzima wa filamu za Kibongo ambapo kwa upande wake alisema anaamini wanaofanya hivyo wanatafuta kuwa mastaa kwa njia ya mkato.
 

“Tatizo ni ulimbukeni wa kuiga wasanii wa nje. Wasanii tunakiwa kujitambua na kufahamu na kulinda utamaduni wetu. Wasanii wengi hawajui thamani zao, jamani ustaa siyo kukaa uchi.
 

“Tujue kuwa kwenye filamu siyo sehemu ya kutafutia mabwana. Kuonesha urembo wetu wa nje na wa ndani kwenye hadhara siyo kitu kizuri kwa utamaduni wetu... hao wanaofanya hivyo wanasababisha wasanii wote tuonekane machangudoa,” alisema Riyama.

Monday, May 20, 2013

NISHA WA BONGO MOVIE AWATALEKEZA WATOTO YATIMA




MSANII wa maigizo, Salma Jabu ‘Nisha,’ amedaiwa kuwatosa watoto yatima waliokuwa wakimsubiri baada ya kuweka ahadi kuwa angekwenda kuwatembelea na kuwapa msaada. 


Tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo Nisha aliahidi kwenda kuwapa msaada watoto yatima wa kituo cha Hisan Orphan Center kilichopo maeneo ya Mbagala Charambe, jijini Dar lakini ulipofika muda, hakutokea.
 


Rafiki wa karibu na staa huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake, alipoulizwa kulikoni alikiri kutotoa taarifa kwa uongozi wa kituo hicho cha watoto yatima na kudai walikuwa na dharura siku hiyo.

“Kuna tatizo lilitokea ikabidi tughairi. Tunaomba radhi kwa kuwafanya wasubiri sana ila niwaambie kuwa mpango wa Nisha kuwatembelea watoto yatima bado upo palepale,” alisema

MADAM RITA WA BONGO STAR SEARCH ANATIA HURUMA...




Kilichompata Madam Rita kinasikitisha! Ndivyo unavyoweza kusema ukibahatika kumuona the big boss wa Benchmark Production inayoratibu Shindano la Bongo Star SearchRita Poulsen ‘Madam’ anayetembelea magongo baada ya kupata ajali mbaya ya gari.

Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kuwa kimya muda mrefu ikielezwa kuwa alipata ajali hiyo kitambo, Madam Rita alisema kuwa kwanza kabisa anamshukuru Mungu kwani anaamini kila kitu kinachotokea chini ya jua kina sababu yake na hata alipopata ajali hiyo alimshukuru kwa kutoka salama.

 Kabla ya ajali


Madam Rita aliendelea kueleza kuwa ajali hiyo aliipata katikati ya Jiji la Dar  na kusababisha kuvunjika kwa kifundo ‘enka’ cha mguu wa kulia hivyo kumsababishia kutembelea magongo baada ya hospitali kumuwekea ‘hogo’.

“Namshukuru Mungu kwanza kwa kunitoa salama katika ile ajali japokuwa sijapona vizuri,” alisema Madam Rita.

Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kuwa alipopata ajali hiyo alikimbizwa katika Hospitali ya Muhimbili kwenye Taasisi ya Mifupa ya Moi lakini hali ilipokuwa kuwa mbaya alihamia katika hospitali moja ya Kichina ambapo kwa sasa amepata nafuu.