Monday, April 1, 2013

SAKATA LA MTOTO ALIYELAZIMISHWA KULA MBEGU ZA KIUME




Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka tisa (jina linahifadhiwa), amefanyiwa unyama wa kutisha na baba yake wa kambo kwa kunajisiwa, kulawitiwa na kulazimishwa kulamba mbegu zake za kiume.

Mtoto huyo anayeishi mkoani Pwani, imedaiwa ana hali mbaya kiafya kutokana na kudaiwa kufanyiwa kitendo hicho kwa muda wa miaka miwili.

Mwanaume anayedaiwa kufanya unyama huo amefahamika kwa jina la Adam Taliani maarufu kama `Kiredio' (37).

Inadaiwa kuwa baba huyo alikuwa akifanya kitendo hicho mbele ya mama wa mtoto huyo ambaye ni mke wake, akiwatishia kuwaua kwa panga kama watatoa siri hiyo.

Akisimulia mkasa huo, mama mdogo wa mtoto huyo Chiku Selemani alisema vitendo hivyo alianza kufanyiwa na baba yake wa kambo tangu mwaka 2011 wakati mama yake alipoanza kuishi na mwanaume huyo.

Alisema, waligundua unyama huo baada ya mtoto huyo kuanza kusema kwa majirani zao jinsi baba yake anavyomfanyia vitendo hivyo usiku huku mama yake akishuhudia.

"Hapo mwanzo tulikuwa tunasikia kwa majirani kuwa mtoto wetu anasimulia mambo mazito, hata hivyo hatukumuamini sana," alisema Chiku.

Chiku alisema kitu ambacho kinamsikitisha kuona dada yake ambaye ndiye mama mzazi wa mtoto huyo alikuwa akishuhudia jambo hilo na wakati mwingine walikuwa wakiingiliwa kwa zamu yeye na mtoto wake.

GIZA LA UNYAMA

Akisimulia huku akimwaga machozi, mtoto huyo ameliambia NIPASHE kuwa baba yake alianza kumuingilia wakati walipohamia kijiji cha Soga, Wilaya ya Kibaha mwaka 2011.

Alisema siku moja usiku wakati amelala, alimuona baba yake akimshika na kumlazimisha kumuingilia huku akimtisha kumkata kwa panga endapo atapiga kelele.

Alisema, aliogopa sana, alimuacha baba yake afanye anavyotaka na hapo ndipo ukawa mlolongo wa kufanyiwa unyama huo kila siku.

"Anaponiingilia napata maumivu makali, nataka kupiga kelele lakini naogopa ataniua kwa panga," alisema mtoto huyo.

Mtoto huyo alizidi kusema kwamba kwa kuhofia kuendelea kufanyiwa vitendo hivyo, aliamua kutoroka nyumbani kwao kila siku nyakati za jioni na kwenda kwa majirani, lakini wazazi wake walimtafuta na kumrudisha nyumbani.

Kutokana na kutoroka mara kwa mara, uongozi wa kijiji hicho uliamua kuwafukuza kijijini hapo na walirudi Mwandege mwishoni mwa mwaka huo.

"Tuliporudi baba alizidi kuniingilia, sasa ilikuwa anafanya kwa zamu, akitoka kwa mama anakuja kwangu na kuniingilia sehemu zote za siri," aliongeza kusema.

MAMA ASAIDIA KUEPUSHA KUNYIMWA UGALI

Hata hivyo alisema wakati anafanyiwa matukio hayo, mama yake anakuwa akishuhudia, wakati mwingine anamsihi asikatae anapoingiliwa kwa sababu watakosa chakula.

"Kila kitu ninachofanyiwa mama anakiona, nipapokataa mama ananiambia nisifanye hivyo ili tuendelee kula ugali wa baba," alisema mtoto huyo.

Alisema kutokana na kufanyiwa vitendo hivyo anaona sehemu zake za siri zimeharibika kwa vidonda.

ALAZIMISHWA KULA MBEGU ZA KIUME


Katika jambo la kusikitisha zaidi, mtoto huyo kabla na baada ya kuingiliwa hulazimishwa kula mbegu za kiume za baba yake ili kumsafisha.

Alisema, wakati baba yake anapomaliza kufanya mapenzi na mama yake, humfuata na kumwambia alambe mbegu zote, kisha anamuingilia mtoto huyo na anapomaliza humlazimisha tena kumsafisha kwa kumlamba.

NDUGU WAINGILIA KATI


Mama mdogo wa mtoto huyo, Chiku alisema baada ya kupata taarifa hizo, walilifikisha suala hilo ngazi ya ofisi ya kitongoji, kijiji na kituo cha polisi kwa ajili ya kumsaidia.

Alisema kwa kushirikiana na polisi wa kituo hicho, alifanikiwa kumpeleka Hospitali ya Wilaya ya Temeke, ambapo huko ilibainika mtoto huyo ameathirika na magonjwa ya zinaa.

Chiku alisema kwenye vipimo hivyo, iligundulika tumbo lake limejaa uchafu na alipatiwa huduma ya kumuondoa uchafu.

"Walinishauri kutokana na afya ya mtoto kuwa mbaya, nimpeleke hospitali ya karibu ya Mkuranga, huko atapewa huduma zote kulingana na magonjwa aliyokuwa nayo," alisema.

Alisema kutokana na kuwa peke yake katika suala hilo, hakuweza kuendelea nalo na badala yake aliliacha na kuendelea kuishi na mtoto huyo katika hali ngumu.

Chiku alisema hawezi kumlaumu sana dada yake, kwa sababu ana matatizo ya akili, ndio maana mwanaume huyo anaweza kufanikisha mambo yake bila kizuizi.

Alisema kutokana na maisha magumu anayoishi, hawezi kushughulikia tatizo hilo na mtuhumiwa kuchukuliwa hatua, aliomba watu binafsi mashirika mbalimbali ya haki za binadamu kuingilia kati.

Pamoja na hayo, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Pwani, Urich Matei, alipoulizwa suala hilo, alisema bado hajalipata, akamuomba mwandishi asubiri ufafanuzi baada ya kupata taarifa kutoka Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mkuranga.

"Taarifa hiyo sijaipata, ni mpya kwangu nakuomba niwaulize wenzangu wa Mkuranga na baadae nitakupatia ufafanuzi," alisema Kamanda Matei.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwandege Ally Ubuguyu alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alithibitisha kutokea.

Ubuguyu alisema baada kupata taarifa hizo, wametoa taarifa katika kituo cha Polisi Vikindu, lakini mpaka sasa hakuna hatua zilizochukuliwa.

"Mtuhumiwa bado yupo hapa kijijini, lakini hakuna polisi aliyekuja kumkamata pamoja na kutaarifu juu ya tukio hili," alisema.

Alisema uongozi wake upo tayari kutoa ushirikiano wa aina yoyote kwa Polisi watakaokwenda kumkamata mtuhumiwa huyo, kwani kitendo alichokifanya ni kibaya.

WALIOFUKIWA NA KIFUSI KWENYE MGODI WA MORRUM JIJINI ARUSHA YAFIKIA 20




WATU zaidi ya 20 wamefariki dunia kwa kufukiwa na kifusi wakati wakichimba  mchanga aina ya Moramu katika machimbo  yaliyopo Moshono nje kidogo ya jiji la Arusha.


Tukio hilo ambalo limegubikwa na simanzi na vilio kwa ndugu jamaa na wananchi, limetokea leo majira ya saa 5 asubuhi wakati marehemu hao wakichimba na kupakia Moramu hiyo kwenye magari .


Pamoja na vifo hivyo magari mawili aina ya Fuso na Scania yameharibiwa vibaya baada ya kufukiwa na kifusi kilichoporomoka umbali unaofikia mita 50 kutoka usawa wa bahari.


Tayari kikosi cha uokoaji ambao ni  Jeshi la Wananchi Kambi ya Tanganyika Parkers kimefanikiwa kuopoa miili ya marehemu 16 waliofukiwa.


Baadhi ya miili ya marehemu  imetambulika kwa majina kuwa ni  Alex Maliaki, Gerald Hamis, Sauli Rafael (Mbu), Barick Loselian, Kababuu Lowasale, Mwenda Kibobori, Japhet Mjivaine na Garald Masai.


Taarifa za mashuhuda zimebainisha kwamba chanzo cha kuporomoka kwa kufusi hicho ni mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Arusha zilizosababisha kukatika kwa Ngema baada ya kuzidiwa na maji ya mvua.

JUMA NATURE AIBUKA MFALME WA TEMEKE BAADA YA KUMFUNIKA VIBAYA TEMBA NA CHEGE




Kundi la wasanii machachali la muziki wa kizazi kipya TMK Wanaume Halisi linaloongozwa na Juma Nature lenye maskani yake Temeke Jijini Dar es Salaam limeibuka kidedea na kuwa mfalme wa Temeke baada ya kulibwaga kundi la Tmk Wanaume Famili katika mpambano wa kumtafuta mfalme wa Tmk lililofanyika jana katika ukumbi wa Dar live Mbagara jijini Dar es Salaam

Juma Nature ambaye ndiye kiongozi wa kundi hilo aliibua hisia za mashabiki wake baada ya kupanda raundi ya kwanza na ngoma aina ya mchiriku huku akisindikizwa na baadhi ya wasanii wanaounda kundi hilo

Akizungumza katika shoo hiyo Nature alisema kuwa aliamini kundi la Tmk wanaume hawataweza kufika round ya pili katika mpambano huo kutokana na uzoefu aliokuwa nao katika fani hiyo

"Aibu yao aibu yao, wamekuja wenyewe hapa ni tatu bila hawafiki round ya pili hao sasa hivi watatoka wenyewe sisi ndio baba zao" alisema Nature
Kundi la Tmk wanaume halisi wakiwa nyuma ya stage teyari kwa kupanda jukwaani kuanza round ya kwanza ya mpambano wao waliingia jukwaani kwa mtindo wa mchiriku


Dogo Lina akiwasalimia mashabiki waliohudhuria pambano hilo yeye aliongoza mpambano wa round ya kwanza na kusababisha kujizolea mashabiki

NATURE NDIYE MFALME WA TEMEKE AWAFUNIKA VIBAYA TEMBA,CHEGE NA KUNDI LAO TAZAMA ILIVYOKUWA


.

Top Talent
Sir Kassim Juma Nature, kinara wa kundi la TMK Wanaume Halisi akiwanyooshea Mike mashabiki wake usiku wa kuamkia leo katika mchuano wa NANI MFALME ambapo mashabiki walimkubali kuwa Mfalme wao dhidi ya mahasimu wao, TMK Wanaume Family.
Mhe. Temba akicheza na mashabiki katika mpambano huo wa kukata na shoka
Sir Nature (kulia) na Doro..kazini