Friday, May 31, 2013

MABADILIKO KUHUSU MAZISHI YA NGWEA



Habari kutoka kwa wanakamati wa mipango ya mazishi ya marehem Albert Mangwea zinasema kuwa mwili wa marehem Ngwea utafika Dar siku ya jumapili saa nane mchana na sio jumamosi kama ilivyoarifiwa hapo awali…


Mwili huo utaagwa siku ya jumatatu saa mbili mpaka saa sita machana ambapo safari itaanza kuelekea Morogoro kwa ajili ya mazishi

KIJANA ANUSURIKA KUFA BAADA YA VIBAKA KUMCHOMA MOTO HUKO MKOANI LINDI



Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ismai Mayoba(31) anayefanya kazi Bar ya Mangrove,Mkazi wa Manispaa ya Lindi amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kundi la Vijana waliotaka kumpora na hatimae kumchoma moto. 

Kwa sasa kijana huyo amelazwa katika Hospital ya Sokoine Mjini humo.

Kufuatia tukio hilo,Jeshi la Polisi wilayani Lindi limefanikiwa kumkamata mtu  mmoja kati ya watuhumiwa saba waliohusika na tukio hilo lilitokea katika eneo la Mtaa wa Congo.


Akithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kukamatwa kwa mtuhumiwa,Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi,Renatha Mzinga alimtaja ndugu Ally Manially(22)mkazi wa mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa na Jeshi hilo na atafikishwa mahakamani leo kujibu shitaka la kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia ya Udanganyifu ikiwa pamoja na kumchoma mwenzie Moto huku akijua ni kosa kisheria.

Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea kutafuta watuhumiwa wengine 6 waliohusika na tukio hilo

ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU NDOA ZA JINSIA MOJA.....UKINASWA IMEKULA KWAKO ( MIAKA 30 JELA )




Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imetunga sheria ya kupiga marufuku ndoa za watu wa jinsia moja.Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Bwana Abubakar Khamis Bakar, aliyasema hayo kwenye Kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi, Saleh Nassor Juma kutoka Chama cha Wananchi (CUF).

Katika swali lake, Bw. Saleh Nassor Juma alitaka kujua ni lini Serikali ya Zanzibar itatunga sheria ya kukataza ndoa hizo na kuweka adhabu kali kwa watu ambao watabainika kufanya vitendo hivyo vichafu. 


Waziri Abubakar amesema, ndoa za watu wa jinsia moja ni kinyume na utamaduni wa Zanzibar na kwamba sheria hiyo imeweka adhabu ya kifungo cha miaka saba kwa wale wote watakaopatikana na hatia hiyo.

Pia alisema kama ninavyomnukuu: "Sheria hii inahusu makosa mengi yakiwemo ya ubakaji, zinaa, usagaji na umalaya ambayo yote yana adhabu ya kifungo cha maisha au miaka isiyopungua 30 gerezani," mwisho wa kunukuu.

HUYU NDO MSHIRIKI WA BBA KUTOKA ZIMBABWE ALIYE CHEZA MKANDA WA NGONO.....WANANCHI WAMEJIPANGA KUMNG'OA



Mshiriki wa shindano la Big Brother Africa Chase kutoka nchini Zimbabwe Nare Pokello amejikuta katika kashfa kubwa baada ya mkanda wake wa ngono kuvuja siku chache tu baada ya yeye kuingia ndani ya jumba la BBA.

 kashfa hiyo ambayo sasa ndio habari ya mjini imezagaa  katika  kurasa kadhaa za Facebook huku mashabiki wengi kutoka nchini kwake wakisistiza watu wampigie kura ya kumng'oa  Pokello nje ya jumba hilo  . 

Mashabiki hao wametengeneza ukurasa hivi karibuni, ambao unashinikiza watu wapige kura za kumng'oa Pokello katika jumba hilo la BBA, Ukurasa huo ulioundwa wiki hii mpaka sasa tayari una zaidi ya wafuasi zaidi ya 4 000.
Katika video hiyo ya ngono, Pokello na mpenzi wake "Desmond Chideme " maarufu kama Stunner wanaonekana wakifanya ngono bila kutumia kinga.

Video hiyo ambayo ilirekodiwa kwa kutumia simu ya iphone na kubadilishwa kwenda kwenye fomati ya avi ilivuja baada ya boyfriend wa pokello kuitoa video hiyo na kumpa rafiki yake wa karibu huku akijisifu.

Katika video hiyo, Stunner anaonekana akizungumza mbele ya kioo cha kamera huku Pokello akiwa anatabasamu. 


video mwishoni inamwonyesha, Pokello akiwa ana ananyonya uume wa Stunner huku Stunner akisema 'wewe msichana ni kituko'.

Chanzo kimoja kilisema Pokello alivujisha video yake mwenyewe na kudai kama siyo yeye aliyevujisha ni Kwa nini alikubali kufanya hivyo kama hawakuwa na nia ya watu kuiona?