Sunday, March 31, 2013

MIILI YA WATU ILIYOPATIKANA KWENYE GHOROFA LILILOANGUKA DAR IMEFIKIA 21 MPAKA SASA



Miili ya watu iliyoopolewa kutoka kwenye vifusi vya jengo lenye ghorofa 16 lililoanguka jana katikati ya jiji la Dar es Salaam, imefikia 21. 
BGkNxjCCQAEyljV
Shughuli za uokoaji zilizoanza jana bado zinaendelea kwa siku ya pili huku kukiwa na taarifa za kuwepo miili zaidi kwenye vifusi hivyo.

Jana Rais Jakaya Mrisho Kikwete alitembelea katika eneo la jengo hilo lililoporomoka lililopo Mtaaa wa Indira Gandhi/Morogoro.
BGhTCALCEAA5EUX
BGhxvZyCAAACKUS
BGj2L20CcAAk2Qh
BGk_iPYCMAA0JzE
BGkGOFQCAAAxCuR
BGkHMJ2CYAAqKHE
BGkhNw7CAAA6hR1
BGkOUrrCIAAEF5U
BGlcQBeCUAA_li0
BGlhHCDCAAEk1YB
BGlHo3LCAAEzet7
BGlKKpQCEAAD_Nd
BGlNk-ACMAIQnCd
BGlTF1nCQAEJ5Sx
BGlTUDmCAAAtzar
BGlvUhpCEAAbSNA

MAHAKAMA YASEMA Uchaguzi Kenya ulikuwa huru na wa haki





Willy Mutunga rais wa mahakama ya juu zaidi Kenya
Mahakama ya juu zaidi nchini Kenya, imeamua kuwa rais mteule Uhuru Kenyatta atasalia kuwa rais mpya wa Kenya baada ya kusema kuwa uchaguzi ulifanywa kwa njia huru na ya haki.
Uchaguzi wenyewe ulifanyika tarehe nne mwezi Machi, ambapo hesabu ya kura ilimpa ushindi Kenyatta kwa zaidi ya laki nane.

Rais wa mahakama hiyo jaji mkuu Willy Mutunga alisema kuwa mahakama imekubali kwa kauli moja kuwa uchaguzi ulifanywa kwa njia ya huru na wazi na kuwa Kenyatta na mgombea mwenza wake walichaguliwa kihalali.

Uamuzi huu una maana kuwa Uhuru Kenyatta ndiye ataapishwa kama rais mpya wa Kenya tarehe tisa mwezi ujao
Kesi hiyo iliwasilishwa katika mahakama ya juu zaidi na mpinzani mkuu wa Kenyatta, Raila Odinga baada ya uchaguzi uliofanyika mapema mwezi huu.


Matokeo rasmi yalionyesha kuwa Uhuru alishinda uchaguzi kwa kumpiku Raila kwa asilimia 50.07 huku Raila akipata asilimia 43.28. Matokeo haya yalizuia kufanyika kwa duuru ya pili ya uchaguzi kwa kura 8,100.


Bwana Odinga aliishutumu tume huru ya uchaguzi na mipaka kwa kuhujumu matokeo ya uchaguzi ili kumpa ushindi Uhuru Kenyatta.


Uchaguzi wa urais, wabunge na wajumbe wengine wa serikali, ulifanyika tarehe nne mwezi Machi, ukiwa wa kwanza tangu uchaguzi uliokumbwa na ghasia mwaka 2007 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya elfu moja.


Bwana Kenyatta na mgombea mwenza wake ,William Ruto,wanakabiliwa na kesi katika mahakama ya jinai kwa kuchochea ghasia za mwaka 2007. Hata hivyo wamekanusha vikali mashtaka.


Mahakama ya juu zaidi inaweza kuthibitisha ushindi wa Kenyatta au kuubatilisha uamuzi wa wakenya na hivyo kuitisha uchaguzi mpya.Vyovyote matokeo yatakavyokuwa kuna wale watakaoghadhabika mno.


Rais anayeondoka mamlakani, Mwai Kibaki amewataka wakenya kuwa watulivu na kukubali uamuzi wa mahakama lakini wengi wanatagemea sana idara ya mahakama ambayo imekuwa na mageuzi makubwa na ambayo sasa watu watu imani nayo.


Mawakili wa Odinga wanasema kuwa kesi yao ilihusisha madai ya kuhujumu hesabu ya kura pamoja na matatizo ya usajili wa wapiga kura na vile vile matatizo ya mitambo ya usajili wa wapiga kura.


Mnamo Ijumaa mahakama ya juu zaidi ilidurusu matokeo ya kura katika vituo 22 vya kupigia kura. Na pande zote mbili zilisema matokeo yalithibitisha misimamo yao.


Kenyatta ameutaja uchaguzi huo kama ishara ya kukuwa kwa demokrasia Kenya na ulifanywa kwa njia ya amani.


Tume ya uchaguzi, pia imesisitiza kuwa uchaguzi ulikuwa huru licha ya hitilafu za kimitambo....


Wachunguzi wa kimataifa nao walisema kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki na kuwa tume huru ya uchaguzi uliendesha uchaguzi huo kwa uwazi.

HIZI NDO PICHA ZA MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRI- ZANZIBAR




 Hapo ndio tujue kuwa wenzetu hawabahatishi na hawana siasa kwenye kazi zao proffessional....kazi kweli kweli!!wamehadithiwa tu wamemchora mtu yule yule!!Angalia Mchoro wa Polisi Hapo chini na Ufananishe na mtu Huyu..


KIJANA AAMUA KUCHOMA MOTO KITAMBULISHO CHA TAIFA CHA KENYA MARA BAADA MAHAKAMA KUHALALISHA USHINDI WA KENYATTA HAPO JANA




Kijana ROBERT STEPHENE OKELLO mwenye asili ya Luo ameingia matatani mara baada ya kuamua kuchoma kitambulisho chake cha Utaifa mara baaada ya mahakama kutengua Pingamizi la Mgombea kupitia Tiketi ya  ODM bwana RAILA ODINGA kupinga Uchaguzi huo.

Kijana huyo aliamua kufanya hivyo kutokana na kile alichokiita kuwa ni Uonevu wa kisiasa na hivyo kupelekea kukichoma kitambulisho hicho ambacho kikatiba ni mali ya Jamhuri ya watu wa Kenya.

Hata hivyo Mahakama Nchini humo haijazungumza kitu chochote mpaka sasa na kuna wasi wasi mkubwa kuwa huenda pakatokea hali ya hatari zaidi kama mahakama itachukua Uamuzi wa kumtia mbaroni kiajana huyo

TASWIRA YA UOKOAJI UKIENDELEA KATIKA AJALI YA JENGO LA GHOROFA 14 LILILOPOROMOKA DAR NA KUUWA WATU KADHAA



Jengo la Ghorofa 14 lililokuwa likiendelea kujengwa pembeni kabisa mwa Msikiti wa SHIA Mtaa wa INDRA GHAND na Zanaki, limeporomoka na kusambaratika na kusababisha vifo vya watu kadhaa ambao hadi sasa idadi haijaweza kupatikana kutokana na waokoaji kukosa vifaa vya kutosha katika zoezi hilo la uokoaji. Imeelezwa kuwa ghorofa hilo limeporomoka leo asubuhi majira ya saa moja na nusu ambapo ulianza kusikika mlio kama 'Tetemeko la ardhi'.
Aidha imeelezwa kuwa katika Jengo hilo walikuwepo mafundi ambao walikuwa wakiendelea na ujenzi na chini alikuwepo Mama Lishe, aliyekuwa akiuza chai na eneo hilo pia walikuwapo watoto wadogo ambao haikuweza kufahamika idadi yao waliokuwa wakicheza eneo hilo, ambao wote inasemekana wamefukiwa na kifusi cha ghorofa hilo, huku waokoaji wakifanikiwa kumpata mtoto mmoja tu ambaye hata hivyo imeelezwa hali yake ilikuwa ni mbaya na kuwahishwa hospitali.
Ni moja ya Kifaa pekee kilichokuwepo eneo hilo Trekta, likifukua kifusi ili kuokoa watu wanaodaiwa kufukiwa na kifusi hicho.
Baadhi ya watu waliwahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha.
Wahindi nao walikuwapo kutoa msaada hapa wakilielekeza Trekta kusogea mahala walipo wao wakihisi kuwa kuna mtu mahala hapo.
Waokoaji wakijitahidi kutumia mikono kuondoa kifusi hicho ili kuweza kuwaokoa watu waliofukiwa.
Trekta likiendelea kuondoa kifusi hicho.
Waokoaji wakiwa hoi......
Juhudi zinaelekea kulala.........
Moja kati ya magari yaliyokuwa eneo hilo likiwa limeangukiwa na mabaki ya jengo hilo.
Trekta likiendelea kuondosha kifusi......../
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik, akihojiwa na wanahabari kuhusu tukio hilo.
Moja ya ghorofa lililo karibu kabisa na jengo hilo lililoanguka nalo likiendelea kujenga nalo pia likiwa na ghorofa 14.....
Sehemu ya wananchi wakishuhudia tukio hilo.
Vijana wakishusha mitungi ya gesi ili kuwasaidia kukata nondo.... baada ya kuona vimekosekana vifaa vya haraka

TASWIRA YA UOKOAJI UKIENDELEA KATIKA AJALI YA JENGO LA GHOROFA 14 LILILOPOROMOKA DAR NA KUUWA WATU KADHAA



 


Jengo la Ghorofa 14 lililokuwa likiendelea kujengwa pembeni kabisa mwa Msikiti wa SHIA Mtaa wa INDRA GHAND na Zanaki, limeporomoka na kusambaratika na kusababisha vifo vya watu kadhaa ambao hadi sasa idadi haijaweza kupatikana kutokana na waokoaji kukosa vifaa vya kutosha katika zoezi hilo la uokoaji. Imeelezwa kuwa ghorofa hilo limeporomoka leo asubuhi majira ya saa moja na nusu ambapo ulianza kusikika mlio kama 'Tetemeko la ardhi'.
Aidha imeelezwa kuwa katika Jengo hilo walikuwepo mafundi ambao walikuwa wakiendelea na ujenzi na chini alikuwepo Mama Lishe, aliyekuwa akiuza chai na eneo hilo pia walikuwapo watoto wadogo ambao haikuweza kufahamika idadi yao waliokuwa wakicheza eneo hilo, ambao wote inasemekana wamefukiwa na kifusi cha ghorofa hilo, huku waokoaji wakifanikiwa kumpata mtoto mmoja tu ambaye hata hivyo imeelezwa hali yake ilikuwa ni mbaya na kuwahishwa hospitali.
Ni moja ya Kifaa pekee kilichokuwepo eneo hilo Trekta, likifukua kifusi ili kuokoa watu wanaodaiwa kufukiwa na kifusi hicho.
Baadhi ya watu waliwahi kufika kujaribu kutoa msaada bila mafanikio hapa wakiwa wamekwama baada ya kukosa vifaa vya kutosha

BREAKING NEWSSSS!! RAIS KIKWETE AMFUTA KAZI MKUU WA MKO WA DAR ES SALAAM BAADA YA JENGO LA GOROFA KUMI NA SITA KUANGUKA.



Rais Jakaya Kikwete

Habari zilizotufikia hivi punde kutoka vyanzo vyetu vya habari, Rais Kikwete amemfukuza kazi Mkuu wa Mkoa wa jiji la Dar es salaam Said Meck Sadick kutokana na uzembe wa kutosimamia kikamilifu ujenzi holela ambao unafanywa na wakandarasi ambao hawana sifa jijini Dar es salaam. Uamuzi huo Rais ameutangaza usiku huu muda wa saa 6.15 leo tarehe 1/04/2013 na kuiacha nafasi yake ya ukuu wa mkoa ikikaimiwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi mpaka hapo atakapo mtangaza Mkuu wa mkoa mwingine.

Sambamba na Mkuu wa Mkoa, Rais amemsimamisha kazi Msimamizi wa Mkoa katika Idara ya Ujenzi sanifu, pamoja na maafisa wawili ambao ni wakaguzi wa majengo wakati yanapokuwa yanajengwa.

Hatua hiyo ya Rais imekuja kutokana na Jengo lenye Gorofa 16 kuanguka na kuonekana uongozi wa juu kuto kuwa na taarifa zozote juu ya ujenzi wa jengo hilo ambalo halikuzingatia vigezo ambavyo vimewekwa kwa ajili ya ujenzi huo, kimoja wapo ni kile ambacho kilitaka ujenzi huo kuishia gorofa 12 na mkandarasi kujenga mpaka gorofa 16. Mheshimiwa Rais ameagiza wale wote ambao wamehusika katika kufanya uzembe wa ujenzi huu wachukuliwe hatua stahiki kulingana na kosa husika. Mpaka hivi sasa ni maafisa kadhaa wameshakamatwa akiwemo mkandarasi ambaye alikuwa analijenga jengo hili.

Kwa kutambua leo ni Tarehe 1 mwezi wa nne tunaamini unaweza ukatambua Rais amechukua maamuzi ambayo ni sahihi ili kuweza kujenga heshima kwa watendaki wake na iwe mfano kwa wengine.
Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

1/04/ 2013

RAPPER CYRILL KID KAMIKAZI AMEFIWA NA MAMA YAKE MZAZI


Top Talent


RAPPER CYRILL KID KAMIKAZE AMEFIWA NA MAMA YAKE MZAZI MAMA JANE KITAINDA. MSIBA UPO TEGETA NYUMBANI KWAO CYRIL. TOP TALENT INATOA POLE KWA FAMILIA ,NDUGU NA MARAFIKI KWA UJUMLA.