Saturday, March 8, 2014

DUNIA SI MDA MREFU ITACHOMWA MOTO!! WAZUNGU WAZIDI KUSAMBAZA LAANA ZAIDI YA SODOMA NA GOMORA.

mwanaume akioa mke zaidi ya mmoja.Yaani kwao wanaona ni haramu sana kuruhusu hilo kwa wanaume.

Lakini cha ajaabu ni kwamba wanaruhusu ndoa za jinsia moja mfano mwanaume kumuoa mwanaume au mwanamke kumuoa mwanamke mwenzie.

Ndoa hizo za jinsia moja zinawezwa kufungishwa makanisani au taasisi zingine zinazohusika na zikaonekana za kawaida sana kwao.
Sasa kama mwanaume kuoa mke zaidi ya mmoja kwa wazungu sio sahihi na wanapinga sana hili,kwanini waone sahihi na kuruhusu ndoa za jinsia moja??

Kama ndoa ya mke zaidi ya mmoja,kanisa au taasisi nyingi za kwao haziwezi kupitisha,yaani mwanaume akawa na wake wawili woote kwa wakati mmoja,kanisa halitaweza kukubali na kufungisha ndoa hiyo maana itaonekana kinyume na taratibu,sasa iweje ndoa za jinsia moja zikubaliwe na kanisa au taasisi hiyohiyo??


Ukienda kwenye maandiko aidha ya biblia au Quran,MUNGU hajaruhusu kabisa ndoa za jinsia moja,sasa hawa wazungu na wote wanazozitetea wanafungisha kwakupitia maandiko gani??? 
Mnaita haki za binadamu,kwanini ndoa za mke zaidi ya mmoja nazo mnazikataa,na hamsemi kuwa ni haki za binadamu bali kwa Africa inaonekana kwamba ndio tuna maadili potofu???
 
Hizi ni zaidi ya laana za Sodoma na Gomora maana kipindi kile zilikuwa zaidi miji hiyo miwili lakini sasa ndoa za jinsia moja zinapigiwa debe zienee dunia nzima kwa kisingizio kwamba ni haki za binadamu.
 
Tanzania tunajipangaaje kukataa ndoa hizi???
 


ANGALIA PICHA ZA KUSHANGAZA ZA NDOA YA JINSIA MOJA KWELI DUNIA IMEKWISHA. 


Mashoga na Wasagaji wamefunga ndoa iliyoshuhudiwa na mamia ya watu katika Kisiwa cha Rhodes Island na Minnesota nchini Marekani.
 

UKISTAAJABU YA MUSA, UTAYAONA YA FIRAUNI…


Ripoti mbalimbali Agosti Mosi mwaka jana nchini Marekani, zinasema kuwa kwa sasa nchini Marekani zaidi ya robo ya Wamarekani wanaunga mkono ndoa za jinsia moja na makanisa mbalimbali yameingia na kuendelea kufungisha ndoa za aina hiyo.

No comments:

Post a Comment