Wednesday, March 27, 2013

HADEMA WAPOKEA MSAADA WA MILIONI 400




Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepokea msaada wa fedha shilingi milioni 400 kutoka Chama cha Upinzani nchini Denmark cha Conservative People’s Party (CPP), kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa kuwajengea uwezo vijana pamoja na Wanawake Viongozi wa chama hicho.

Akizungumza wakati wa kutiliana saini Mkataba wa utekelezaji wa Mradi huo, Katibu Mkuu wa CHADEMA, DK. WILBROAD SLAA amesema awamu ya kwanza ya utekelezaji wa Mradi wa kuwajengea uwezo Wanachama wake kupitia Baraza la Vijana la Chama hicho, (BAVICHA), pamoja na lile la Wanawake (BAWACHA), inatarajiwa kuanza Machi, mwaka huu.


Kwa upande wake Mwakilishi wa Chama cha Conservative People’s Party (CPP), ROLF AAGAARD, anaelezea lengo la chama hicho kutoa msaada huo.


Nae Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (CHADEMA), JOHN HECHE amesema msaada huo utawawezesha kutoa mafunzo kwa Viongozi wa Baraza hilo katika mikoa mbalimbali nchini.


Chama cha Conservative People’s Party (CPP), kilianzishwa mwaka 1915 na kimekuwa madarakani kwa kipindi kirefu hadi kiliposhindwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita nchini

HUU NDO UTAJIRI WA WEMA SEPETU..... CHEZEIYA WEMA WW!!!!!




Well, well, well! Hiki ni kitu ambacho kila mmoja anapenda kukifahamu. Wema Sepetu ni tajiri kiasi gani? Ni ngumu kusema exactly mrembo huyu ana shilingi ngapi benki, lakini mambo anayofanya yanatupa jibu la wazi kuwa, Wema ana mkwanja mrefu. So hebu tuangalie mangapi makubwa yaliyohusisha fedha nyingi aliyoyafanya kuanzia mwezi June, 2012.
IMG_4951
1. Thamani ya nyumba yake
Wema Sepetu aliwaacha hoi watu wengi baada ya kuonesha nyumba yake mpya exclusively kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV. Alisema thamani ya nyumba yake hiyo ilifikia shilingi milioni 400 na hiyo ni tofauti na karibu shilingi milioni 30 za kuipamba ndani. Hiyo ilikuwa ni tarahe za mwanzo za mwezi June, 2012.
Sebule
Sebule

Wema Sepetu akielezea jambo
Wema Sepetu akielezea jambo
Wema na Zamaradi Mketema wa Clouds TV
Wema na Zamaradi Mketema wa Clouds TV
912
Sehemu ya nje ya nyumba
Sehemu ya nje ya nyumba
616
Dj Choka alikuwa miongoni mwa watu waliotembelea nyumba hiyo
Dj Choka alikuwa miongoni mwa watu waliotembelea nyumba hiyo
2. Uzinduzi wa filamu yake Superstar 
Katika historia ya Bongo Movies, hakuna filamu iliyowahi kuwa na uzinduzi wa nguvu kama wa filamu ya Wema ambayo hata hivyo haijawahi kutoka, Supastar. Katika uzinduzi huyo, Wema alimdondosha muigizaji namba moja wa kike nchini Nigeria, Omotola Jalade ambaye alimpeleka kwenye event iliyofanyika Giraffe Hotel Ocean View ambako watu mbalimbali walikutana kubadilishana mawazo na Omotola. Hiyo ilikuwa ni baada ya kushindwa kufika kwa wakati.
IMG_6117
Awali ulifanyika uzinduzi wa filamu hiyo yenye mastaa kibao akiwemo yeye mwenyewe, TID, Shetta, Mwinyi Machozi, Chaz Baba, Barnaba na wengine kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro ambako mastaa wote wa orodha A nchini walihudhuria huku Shaa na Shilole wakiwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza.
DSC_0075
Ben Kinyaiya na Irene Uwoya
Ben Kinyaiya na Irene Uwoya
Ray, Dr Cheni, Steve Nyerere nao walihudhuria
Ray, Dr Cheni, Steve Nyerere nao walihudhuria
DSC_0172

Shughuli nzima hiyo iliyofanyika mwishoni mwa mwezi June mwaka jana, ilitumia takriban shilingi milioni 40 zikiwemo gharama za kumlipa Omotola.

3. Gari anayomiliki
Kwa sasa Wema anamiliki gari aina ya AUDI Q7 ambayo thamani yake inafikia shilingi milioni 80. Awali ya hapo alikuwa na Toyota Mark X ambayo thamani yake ni takriban shilingi milioni 60.
Wema akiwa na mkoko wake
Wema akiwa na mkoko wake
4. Thamani ya ofisi na kampuni yake, Endless Fame Films
February 21, Wema alifanya uzinduzi maalum wa ofisi za kampuni yake ya Endless Fame Films zilizopo Mwananyamala jijini Dar es Salaam ambazo thamani yake ni takriban shilingi milioni 70.
DSC_1824
off12-600x600

5. Gharama anayotumia kuwatunza mbwa wake, Vanny na Gucci

Mtandao wa Global Publisher jana uliandika, “KWA wale wenye hali ngumu kimaisha wataishia kusema; ni kufuru iliyoje kwani staa wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu hivi karibuni amewafanyia mbwa wake wawili ‘shopping’ iliyogharimu dola 4,000 za Kimarekani (zaidi ya Sh. milioni 6.5 za madafu).

Wema aliteketeza kiasi hicho cha fedha kwa kuwanunulia mbwa hao pafyumu, viatu na nguo, alivyoagiza kutoka nchini China, lengo likiwa ni kuhakikisha wanaishi katika mazingira mazuri.

Akizungumzia ‘shopping’ hiyo nyumbani kwake Kijitonyama, jijini Dar, Wema alisema: “Kiukweli nawapenda sana hawa mbwa, ukinipasua roho yangu utawakuta ndiyo maana nataka wavae na kunukia vizuri, kinyume chake siwezi kuwa na amani.
0caeb4ac921811e28e6622000a9f0a1a_7
Vanny na Gucci wakicheza
Vanny na Gucci wakicheza
83b019e2914b11e28e0922000a9f1335_7
818e18e0921c11e2af9022000a1f9a23_7
90197700921811e2996f22000a1fbc6f_7
Vanny
Vanny
Vanny
Vanny
Gucci akiwa amelala
Gucci akiwa amelala

“Najua watu wanaweza kushangazwa na kitendo cha mimi kutumia kiasi hicho cha fedha lakini sioni kama ni tatizo kwani ni kitu ambacho kinanipa furaha katika maisha yangu.”

Leo kupitia Instagram, Wema ameandika, “Vanny ake heading to da hospital…. my poor baby is sick…. nat happy at all, hope u get better soon.”

6. Shilingi milioni 13 alizomtolea Kajala baada ya kusomwa hukumu yake

Jana Wema Sepetu alimake headline baada ya kutoa mfukoni mwake shilingi milioni 13 kulipa faini aliyopigwa muigizaji mwenzie Kajala Masanja aliyehukumiwa jana kwenda jela miaka mitano ama kulipa kiasi hicho cha fedha.

Akizungumza exclusively na Bongo5, Wema amesema hakufikiria mara mbili kutoa kiasi hicho cha fedha.
“Kusema kweli wanasemaga kwamba kutoa ni moyo so naamini what I did is best, nimetoa kwasababu I had to do it and sikuthink twice kuhusu kufanya hivyo,” amesema Wema.


“Nimefanya kama namsaidia rafiki yangu kama namsaidia ndugu yangu na sidhani kama ingekuwa ni kitu kizuri kumuona mwenzako anaingia kwenye dhahama, kwenye tabu, kwenye mateso na wakati nina uwezo wa kumsaidia kwahiyo I just did what I had to do.”
7. Jinsi anavyomwaga hela kwenye sherehe mbalimbali
Katika katika sherehe za 8020 Fashion’s Woman Celebration zilizofanyika kwenye siku ya wanawake duniani, Wema aliuteka ukumbi wa Diamond Jubilee baada ya kumwaga mihela kwa mwimbaji maarufu wa Taarabu nchini, Khadija Omar Kopa. Wema alimwaga mkwanja huo kumpongeza Khadija kwa kukonga moyo wake.

Hayo ni machache tu tunayofahamu na kwa hesabu hizo bila shaka utakubaliana nasi kuwa Wema Sepetu ana mkwanja mrefu!!!

ALIYEMGONGA TRAFIKI ENEO LA BAMAGA AFIKISHWA MAHAKAMANI





Akiteta jambo na Issa Mnally  ndani ya mahakama kabla ya hakimu kuwasili. 


  Waandishi wa habari wakimpiga picha (Simbo) wakati akiingia mahakamani...


Akiondoka eneo la mahakama mara baada ya kesi kuahirishwa akiwa na wakili wake.
 Jackson  Simbo anayedaiwa kumgonga kwa gari marehemu trafiki Elikiza Nko wiki iliyopita maeneo ya Bamaga-Mwenge  jijini Dar ss Salaam amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mshitakiwa huyo ameachiwa kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapo tajwa tena Aprili 15 mwaka huu

YULE MTOTO WA MIAKA 8 ALIYEOA BIBI WA MAIAKA 61 ADAI KUFURAHIA FURAHA KUITWA BABA





KUSHOTO: Sanele akibusiana na mkewe, Helen siku ya harusi yao wiki mbili zilizopita. KULIA: Sanele na Helen walipata chakula cha usiku pamoja nyumbani kwa mkewe huyo.

Huku miguu yake ikining'inia juu ya sakafu na sehemu yake ya chakula cha mtoto, inaonekana kama anakula chakula cha usiku na bibi yake.Ukweli ni kwamba Sanele Masilela, mwenye miaka 8, anafurahia chakula cha usiku na mke wake, baada ya kumuoa wiki mbili zilizopita, na inasemekana kwa sasa ameanza kujisikia kama mume kamili.

Mwanafunzi huyo alimuoa Helen Shabangu baada ya mababu zake kuwasiliana naye kutoka nyuma ya makaburini wakimweleza kwamba anatakiwa kuoa.Mwanafunzi huyo alimchagua rafiki wa familia yao na mama wa watoto watano Helen na familia yake ikalipa Pauni za Uingereza 500 kuwezesha mama huyo kuwa mkewe katika sherehe iliyogharimu Pauni 1,000 mjini Tshwane, Afrika Kusini.

Sanele alikiri kwamba tangu harusi hiyo, ameanza kujisikia kama mwanandoa.Alisema: "Siku hiyo ilikuwa ya kipekee na hakika ilikuwa kama alivyokuwa akifikiria itakuwa."Marafiki zangu walifikiri ni mzaha kwamba nilikuwa naoa lakini sasa najisikia kama mume."

Akiwa amevalia tai na suti ya rangi ya shaba, Sanele, mtoto wa mwisho katika familia ya watoto watano, alivalishana pete mbele ya wageni 100 na hata kufikia kupigana mabusu na mkewe huyo.Lakini, licha ya muonekano, haikuwa halisia, ndoa hiyo ilikuwa ni kutimia mila na haikufungwa kisheria.

Wanandoa hao hawaishi pamoja lakini Helen mara kwa mara anamwalika kula naye chakula cha usiku pamoja kwenye nyumba anayoishi na familia watoto wake.Sanele amerejea kwenye maisha yake na kuendelea kufurahia shule na kucheza kandanda na marafiki zake lakini anakiri kwamba ndoa hiyo ilikuwa muhimu mno kwake.

Alisema: "Babu yangu aliwasiliana nami kupitia picha ya harusi ya mama yangu."Tuna mahusiano maalumu sababu nimerithi jina lake."Alisema aliona picha hiyo na kujihisi mnyonge kwamba hakuwahi kuweza kufunga ndoa yake mwenyewe hivyo alinitaka mimi nifunge ndoa. Nilimchagua Helen sababu nampenda sana."

Habari za harusi hiyo zimeshitua dunia nzima lakini Helen, ambaye ameshaolewa kwa miaka 30 sasa na kupata watoto watano wenye umri wa kati ya miaka 37 na 27, ametetea sherehe hiyo.Alisema: "Nafahamu habari hiyo imesambaa dunia nzima na kubwa ni kuwa nchi nyingine zimeweza kujifunza kuhusu utamaduni wetu na mababu zetu.

"Tulichofanya hakikuwa makosa. Ni utamaduni wetu tu. Pale mababu zetu wanapoagiza kitu, tunafanya kile wanachosema. Sidhani kama watu wengine wanaelewa hilo."Nafahamu mababu wamefurahi sasa sababu tuko sawa na kila kitu kinaonekana safi."Familia nzima imefurahi sana kuliko ilivyowahi kutokea."

Helen alikiri sherehe hiyo ya gharama ilikuwa kubwa kuzidi ilivyokuwa harusi yake halisi na mumewe, Alfred, mwenye miaka 65, na hakuna cha kujutia.Aliongeza: "Kila mara nitakuwa karibu na familia ya Sanele kuliko ilivyokuwa kabla ya harusi hiyo na kabla Sanele kunichagua mimi kama mkewe tulikuwa karibu mno.
"Hakuna kilichobadilika tangu wakati huo."

Mumewe kwa miaka 30, Alfred mwenye umri wa miaka 65, alisema: "Watoto wangu na mimi tumefurahi.
Sanele pia alisema anatarajia atafunga ndoa sahihi kwa mwanamke wa umri kama wake wakati atakapokuwa mkubwa.

Aliongeza: "Nilimweleza mama yangu kwamba nilitaka kuoa kwa sababu hakika nilikuwa nataka kufanya hivyo."Nimefurahi kwamba nimemuoa Helen - lakini nitaenda shule na kusoma kwa bidii."Pindi nitakapokuwa mkubwa nitaoa msichana wa rika langu."

Mama wa Sanele mwenye miaka 46, Patience Masilela aliongeza kwamba anaamini sherehe hiyo 'haikuwa na tatizo' na kwamba imewatuliza mababu.Alisema: "Hii ni mara ya kwanza kutokea katika familia hiyo."

HUYU NDIYE MKE ANAYELALAMIKA KUIBIWA MUME NA 'JACK CHUZ' ALIYEFUNGA NDOA HIVI KARIBUNI




ZENGWE limeanza! saa 48 baada ya Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ kufunga ndoa na jamaa aitwaye Gadna Dibibi, mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mariam Omary ameibuka na kudai muoaji ni baba mtoto wake wa miezi minne hivyo anamuomba msanii huyo amwachie mumewe. 

Mariam Omary anayedai Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ kamchukulia baba watoto wake akiwa na mwanaye.

 
Kwa mujibu wa chanzo makini, baada ya kuenea kwa habari za Jack Chuz kufunga ndoa na kijana huyo wikiendi iliyopita, ndipo ilipogundulika kuwa ana mwanamke ambaye wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa takribani miaka mitatu na wana mtoto huyo mmoja wa kiume.


Baada ya ripota wetu kuidaka ishu hiyo aliingia mzigoni kutafuta ukweli wa jambo hilo ndipo akakutana na mwanamke huyo aishie Kigogo, Dar ambapo alikutwa akiwa anambembeleza mtoto huyo anayeitwa Price Laden.


Akifunguka mbele ya mwandishi  wetu, Mariam alidai kwamba siku ambayo mwanaume huyo alifunga ndoa (Ijumaa), alimuaga anasafiri kwenda Morogoro hivyo hatakuwepo Dar lakini wanusaji wa mambo ya watu walishampa ‘infomesheni’ kwamba anafunga ndoa na Jack Chuz.


“Unajua mtu atakunyima ugali ila siyo maneno, nilishajua na nilikuwa namwangalia tu nione atasemaje,” alisema.

Mariam aliendelea kutiririka kwamba anamjua vizuri Jack Chuz linapokuja suala la wanaume wa wenzake lakini kwake atachemsha kwa kuwa msanii huyo anajua kila kitu juu ya uhusiano wake na mwanaume huyo ambaye ni halali yake.


“Hakuna asichokijua kati yangu na Dibibi, kwa usalama wake Jack aniachie mume wangu,” alilalama mwanamke huyo.


Baada ya kuzungumza na Mariam, mwandishi wetu alimvutia waya mume wa Jack na kusomewa mashitaka yake ambapo alisema kuwa baba wa mtoto anayemjua ni mama peke yake na isitoshe kuzaa naye isiwe sababu kwani yeye hakumuoa.


“Alikuwa demu wangu na kuzaa mtoto isiwe sababu. Hata hivyo, ukweli wa baba wa mtoto anayejua ni mama. Sikumtolea mahari wala kumvalisha pete ‘so’ hana kizuizi na ndoa yangu,” alisema jamaa huyo kisha akakata simu

SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA LAMMPONGEZA WEMA SEPETU




SHIRIKISHO la Filamu Tanzania (TAFF) limempongeza msanii wa kike Wema Sepetu kwa moyo wa upendo aliouonyesha kwa msanii mwenzie Kajala Masanja kwa kumlipia faini ya sh. milioni 13 alizotozwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutokana na kupatikana na hatia katika kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa inamkabili mahakamani hapo

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wengine rais wa shirikisho hilo Simon Mwakifwamba alisema kuwa imani na moyo wa upendo aliokuwa nao msanii Wema ndio uliomsukuma kumlipia kiwango hicho cha fedha bila ya kujiuliza mara mbili kitendo hiko kimeonyesha jinsi gani wanavyohitaji kushirikiana katika matatizo

Alisema kuwa wasanii wanatakiwa kujifunza kutoka kwake kwani wanahitaji kuwa kitu kimoja kujaliana kwenye matatizo na kutambua kuwa wao ni familia moja wanaojenga nyumba moja

"Kitendo alichoonyesha msanii mwenzetu ni kitendo cha kuigwa na cha kiimani siyo kwamba anauwezo sana hapana ila kujali na utu ndio kilichomsukuma atoe fedha hizo" alisema Mwakifwamba

"Unajua kuwa nacho na kutoa ni vitu tofauti wengi pale walikuwa navyo ila labada hawakuwa na moyo wa kutoa hivyo Wema mungu atambariki na kumuongezea pale alipopunguza " aliongeza Mwakifamba

Mwakifamba alimtaka Kajala kutoa shukurani kwa mungu kwa kumsaidia kumtoa kule alipokuwa kwani sehemu yenye mateso na inayoumiza katika maisha ya kila siku

Wakati huo huo kwa upande wake Msanii Wema Sepetu "Imenichukua masaa mawili kufanikisha hili,nilienda benki nikatoa fedha na kuja hapa kulipa, ni sh.milioni 13".Hii ni kauli ya Msanii wa Filamu Wema Sepetu akizungumza na waandishi wa habari buda mfupi baada ya kukamilisha zoezi la kumlipia faini ya kiasi hicho cha fedha msanii mwenzake Kajala Masanja.

Wema alisema kuwa mumlipia Kajala kiasi hicho cha fedha haoni kama amepoteza kwani msanii huyo ni kama ndugu yake wa karibu.

"Katika vitu vingi sana,kumsaidia kwangu sijaona kama nimepoteza chochote,naona kama nimetoa kitu kama mtu  yoyote anayeweza kufanya hivi kwasababu kutoa ni moyo,sihitaji kulipwa chochote mwenyezimungu ndiye atanilipia"alisema

Aliongeza kuwa "Nahakika hakuna mtu anayependa kukaa gerezani,kwahiyo nimeona kama nitafanya hivyo nitamuokoa katika hali zote mbaya"

Kwaupande wake Dkt.Cheni alimewataka wasanii nchini kuwa na ushirikiano pale mmoja wao anapopatwa na matatizo kwani wao ni kitu kimoja na ni familia moja hivyo kushirikiana kwao ndio kutaendelea kuimalisha undugu walio nao na kufanikiwa katika kazi wanayoikusudia

Alisema katika maisha hakuna mtu aliyewekwa alama usoni kuwa atakuwa wa matatizi tu bali kila mtu anaweza kupata tatizo kwa aina yoyote hivyo tunatakiwa tuwe karibu.

"Kiukweli sina la kusema zaidi kwani matatizo yanamkuta kila mtu na yanapokukuta unakuwa haujajua,Mtu unaweza kuona unafanya jambo sahihihi lakini kijamii au kisheria linakuwa tatizo,ninachoomba kwa wasanii wenzangu tuwe na ushirikiano pale mwenzetu anapopatwa na tatizo kama hili tujitoe kwa mwenzetu"Alisema Dkt.Cheni.

Awali Dk.Cheni alisema kuwa wangeweza kuchangishana kiasi hicho cha fedha na kuzilipa lakini baadaye Wema alionekana akitoka mbio katika viwanja vya mahakama hiyo na kwenda katika gari lake ambapo ilidaiwa alikwenda benki kutoa fedha.

Kajala alitoka gerezani baada ya kulipiwa kiasi hicho cha fedha na msanii mwenzake Wema Sepetu muda mfupi baada ya kusomwa hukumu hiyo.

BINTI WA MIAKA 16 ALAZIMISHWA KUNYWA MKOJO NA MAMA YAKE MDOGO HUKO IRINGA




Vituko mjini Iringa haviwezi kuisha kama jamii haitakubali kwa moyo mmoja kupambana na ukatili wa kijinsia. Huyu ni Binti ZAWAD KARIM miaka 16 mkazi wa mshindo nyuma ya banki ya NBC manispaa ya Iringa amepigwa na hatimaye kunyweshwa mkojo na mama yake mdogo aitwaye Ever ubamba.

Tukio lilikuwa hivi:
Zawadi  kimsingi anaishi na mama yake mzazi ambaye kwa kipindi hicho dada mtu huyo alikuwa anaumwa. Ever alikuwa nje na marafiki zake ndipo mama yake mdogo huyo akamwiita ndani ya nyumba yao hiyo wanayoishi mtaa wa mshindo.

Baada ya kumwita na kisha mtoto huyo kushindwa kusikia baadaye aliitika na kuingia ndani na  ndipo alipo ambiwa avue nguo zote na huyo mama yake  mdogo Ever .Baada ya muda mfupi Zawadi alianza kupokea kipigo kikali kutoka kwa mama yake  mdogo.

Katika kipigo hicho Zawadi  alipigwa pamoja na kunyweshwa mkojo kutoka kwa mama yake mdogo huyo.Zawadi ambaye ni mtoto wa kuzaliwa na Dada yake Ever inadaiwa kipigo hicho kimesababishwa na tuhuma kwamba eti familia hiyo haina mtoto kama yeye zawadi.

Zawadi inadaiwa aliwahi kwenda zanzibar kwa nia ya kufanya kazi na baada ya muda mama yake mzazi ambaye jina lake bado halijafahamika alimpigia simu arudi nyumbani na mara baada ya kurudi ndipo kutokuelewana huko kukajitokeza.

Aidha taarifa za ndani kuhusu tukio hilo zinasema kuwa Mama yake Msichana Zawadi alitupwa akiwa mchanga na kuokotwa na wasamalia wema na hatimaye kulelewa na Bibi yake ambaye hata hivyo amefariki duni.

Kisa cha yote hayo ni madai ya mtoto zawadi kuomba aoneshwe Baba yake mzazi ili walau aweze kupata pumziko la adha anazo zipata kutoka kwa ushirika wa ndugu zake hao.Zawadi pamoja na majirani wameuambia mtandao huu kuwa vitu vilivyo tumika kumwadhibu vilikuwa ni pamoja na nyaya za simu,mkandaa,na vipande vya chupa katika kumchoma navyo.

Hata hivyo hadi mtandao huu unachapisha taarifa hii watuhumiwa wa tukio hili yaani Mama mzazi pamoja na Mama mdogo wa Zawadi wanashikiliwa na jeshi la polisi kitengo cha dawati la jinsia kwa mahojiano zaidi.

HABARI ZILIZOPO KATIKA MAGAZETI YA LEO....



..
.
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
..
.