Sunday, April 28, 2013

Nassari Akiwa na Lema Mahabusu



Kushoto ni Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akiwa katika chumba alikohifadhiwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.Dar es Salaam, Tanzania. Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari LEO amemtembelea Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye yuko mahabusu baada ya kutiwa mbaroni na Jeshi la Polisi, mkoani Arusha, Tanzania.

Nassari pamoja na mambo mengine amemtembelea Lema ili kujua kilichotokea wakati akizungumza na wanafunzi wa Taasisi ya Uhasibu  Arusha (IAA) na baadaye kukamatwa na polisi.

Mbunge huyo Arumeru Mashariki amewasili Leo Arusha na kwenda moja kwa moja katika Kituo Kikubwa Cha Polisi (Central).

Jana Nassari alinukuliwa akisema kwamba Leo yeye na Halima Mdee (Kawe) watakutana na kuzumgumza na Mulongo kuhusu

kilichotokea katika chuo hicho cha uhasibu na kusababisha kukamatwa kwa Lema.

“Jumatatu (leo) tunatarahia kuonana na mkuu wa mkoa na tayari nimempa taarifa. Tunataka kuzungumza  naye kilichotokea na hali ya kisiasa  iliopo Arusha hivi sasa,” alisema Nassari.

Mpaka sasa haijafahamika Nassari amezungumza nini na Lema.

BAJETI KIPORO WIZARA YA MAJI YATINGA TENA BUNGENI LEO





Mkutano wa 11 unaendeleo leo mjini Dodoma, ambapo Bajeti ya Wizara ya Maji iliyokwama kupitishwa baada ya wabunge kuigomea, inatarajiwa kuwasilishwa, ikiwa na  maboresho, hususani eneo la nyongeza ya fedha katika miradi ya maji.

Bajeti hiyo ilitarajiwa kupitishwa tangu Alhamisi wiki  iliyopita, lakini kutokana na ufinyu wa fedha zilizotengwa, takribani wabunge wote waliochangia mjadala wake, wakiwemo wa CCM, waligoma kuiunga mkono.
 
Kutokana na hali hiyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda alisema suala la maji haliwezi kufanyiwa utani na kuitaka Wizara ya Maji, Kamati ya Bajeti na Wizara ya Fedha, kufanyia kazi suala hilo na walete majibu ya uhakika.
 
Leo wabunge hao wanatarajia upande wa Serikali kuwasilisha bajeti hiyo, ikiwa na maboresho mapya ya nyongeza ya fedha za miradi inayotarajiwa kufikia zaidi ya Sh milioni 185, ambazo wabunge hao walipendekeza ili kutekeleza miradi ya maji na kupunguza tatizo la maji katika maeneo yao.
 
Wakati akiiwasilisha makadirio ya bajeti hiyo wiki iliyopita bungeni, Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, alibainisha kuwa Wizara hiyo imetengewa Sh bilioni 398, fedha ambazo wabunge hao walibainisha kuwa hazitoshi, ikilinganishwa na mahitaji makubwa ya maji nchini.
 
Wakati akiahirisha mjadala huo wa Bajeti ya Maji, Spika alisema: “Naona sasa mahitaji ya wabunge wote na wananchi kwa ujumla ni bajeti hii, kwa kweli iboreshwe ili kufikia malengo stahiki katika maeneo yetu.”

Viongozi wa Wizara ya Fedha, Kamati ya Bajeti na Wizara ya Maji, kwa takribani siku tatu, walikutana na kujadili suala hilo na namna ya kupata fedha za kuongezea kwenye bajeti hiyo, huku wabunge wa CCM nao wakikutana ili kuwekana sawa, kutokana na kilichotokea bungeni kuhusu bajeti hiyo.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe, alipongeza hatua za wabunge hasa wa CCM, kuweka itikadi zao pembeni na kuungana pamoja kuikataa bajeti hiyo, ambayo haikuwa na mfumo mzuri wa kumaliza tatizo la maji nchini.
Hata hivyo, alipendekeza leo Serikali ije na maboresho yatakayoainisha namna ya kutekeleza Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo, uliozinduliwa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete, ambao katika eneo la maji utahitaji Sh bilioni 500.

Pamoja na mjadala wa Bajeti ya Maji kuendelea leo, pia Wizara ya Maliasili na Utalii, inatarajiwa kuwasilisha bajeti yake ya mwaka 2013/2014, itakayojadiliwa kwa siku mbili, ambapo wabunge wengi wanatarajia kuzungumzia suala la mgogoro wa ardhi Loliondo.

Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria nayo inatarajiwa kuwasilishwa kesho huku suala la Mabaraza ya Katiba likiwa ajenda kuu, iliyopaniwa kujadiliwa hasa na wapinzani, ambao wamekuwa wakilalamikia mchakato wake wa uchaguzi, kwamba umekuwa ukitawaliwa zaidi na masuala ya siasa.

Katika wiki hii, bajeti nyingine itakayojadiliwa ni ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), ambayo itajadiliwa kwa siku moja.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA TAASISI YA 'CONFUCIUS' YA CHUO KIKUU CHA DODOMA




 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi ya 'Confucius' ya Chuo Kikuu cha Dodoma, ambayo ni maalumu kwa ajili ya kufundishia Lugha na Tamaduni za Kichina. Uzinduzi huo umefanyika jana Chuo Kikuu cha Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti cha kuhitimu mafunzo ya Lugha ya Kichina, mmoja kati ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Jamillah Dauda, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi ya 'Confucius' ya Chuo Kikuu cha Dodoma, ambayo ni maalumu kwa ajili ya kufundishia Lugha na Tamaduni za Kichina. Uzinduzi huo umefanyika jana Chuo Kikuu cha Dodoma. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma, Prof. Idrs Kikula.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipongezana na Balozi wa China nchini Tanzania, Lu Youqing, baada ya kuzindua rasmi Taasisi ya 'Confucius' ya Chuo Kikuu cha Dodoma, ambayo ni maalumu kwa ajili ya kufundishia Lugha na Tamaduni za Kichina. Uzinduzi huo umefanyika jana Chuo Kikuu cha Dodoma. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma, Prof. Idrs Kikula.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo cha Dodoma, Prof. Idris Kikula, wakati akitembele kukagua majengo ya Taasisi ya 'Confucius' ya Chuo Kikuu cha Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kuhusu Lugha na Tamaduni za Kichina, kutoka kwa Mkuu wa Taasisi ya 'Confucius', Zheng Xueyu, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi hiyo ya Chuo Kikuu cha Dodoma.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia michoro ya picha zinazochorwa na wanafunzi wa Taasisi ya Confucius.
 Makamu wa Rais Dkt. Bilal;, akiagana na baadhi ya viongozi wakati akiondoka eneo hilo baada ya uzinduzi rasmi.
 Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akitembelea kukagua ujenzi wa Chuo cha Afya kinachojengwa Chuo Kikuu cha Dodoma.
 Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na viongozi mbalimbali.
Picha ya pamoja.

BUSU SI UGOMVI......MAMBO YA KUIGA YATATUMALIZA




Hawa  jamaa  nadhani  wanahitaji  "kupigwa  pindi"  la  matumzi  ya  midomo  yao  kuhusu  "mabusu"  ambayo  ni  mila  tulizoridhi  toka  kwa  wenzetu...

Kama  hujui  potezea....siyo  lazima  upige  busu....usije  ukamng'ata  mwenzio  bwana.!!!




MUME WANGU HANA PUMZI KITANDANI....KWAKE DAKIKA TATU NI NYINGI SANA....NAOMBENI USHAURI



Mimi ni mdada wa miaka 27 na nina watoto wawili kwa sasa nimeolewa na mkaka mwenye miaka 32.

Kwa kweli mume wangu ni kijana handsome. Katika maisha yangu ya usichana mpaka kuolewa nimekuwa na mahusiano na wanaume takribani 4 kabla ya mume wangu.

Wanaume hao wote kwakweli walikuwa nao wazuri  na kati yao wawili walikuwa waume za watu na walikuwa na maumbile yakunitosha.... 



Pamoja na maumbile  yao,sikuwahi kufika kileleni japokuwa walikuwa wanapumzi ndefu yaani walikuwa wanaweza kuplay for about  1 hour . Tena kama tutalala pamoja usiku huo walikuwa wanaweza hata 4-5.

Nilipompata mume wangu nilimpenda toka rohoni na baada ya mhusiano ya miaka miwili tulioana,tatizo ambalo lipo kwenye ndoa yangu na nililiona toka mwanzo ni kwamba mume wangu hana pumzi kitandani japokuwa ndio mwanaume pekee anayenifikisha kileleni .

Yaani mume wangu yeye ni 3 minutes tu amemaliza  na baada ya muda anakoroma, hatuwezi kufanya hata mara  mbili kwa usiku hata nikimchezea anashindwa kusimama labda afanye kimoja asubuhi kingine usiku.

Na ili nikojoe kuna staili lazima niziapply mimi mwenyewe niwe najigusa kwake maana yeye tukifanya anashindwa kujizuia mara moja anakojoa.

Nisaidieni wapendwa nifanyaje maana  bado  nampenda  mume  wangu."
---------------


Jibu la Dyna: 

Shukurani sana kwa ushirikiano, hongera kwa kufanikiwa kufika kileleni kwani sio wanawake wote hufika hapo. Sidhani kuwa ni kweli kuwa mumeo anakojoa ndani ya dakika 3 na wakati huohuo wewe unafika kileleni.

Unapokuwa kwenye uhusiano wa kudumu au ndoa hupaswi kabisa-kabisa kurudisha mawazo yako nyuma na kuanza kufananisha utendaji wa wanaume uliokuwa nao na mpenzi wako wa sasa/mumeo. Jifunze kukubali jinsi mumeo alivyo na ridhika na uwezo wake aliojaaliwa na Mungu.

Ndio maana kabla ya uchumba kutangazwa kule kwetu huwa kuna swali unaulizwa na mama au bibi au shangazi


- "je una uhakika kuwa unataka kuolewa na huyu bwana? 


-je uko radhi kuishi nae hata kama siku moja utagundua kasoro zake? (kasoro hapa wanamaanisha kushindwa kufanya tendo). 


Hivyo basi unapofunga ndao na mtu na kugundua kuwa uwezo wake kitandani umebadilika ghafla kutokana na umri au mataizo mengine ya kiafya, unatakiwa kukubali tatizo na kumpa ushirikiano ili kuepusha matatizo.

Kilele na mwanamke:
Mwanamke anafika kileleni kuanzia Dk 10 mpaka dk 45 tangu tendo lianze na pengine inaweza kuchukua muda mrefu zaidi, hivyo basi kama unafanikiwa kufika kileleni ni wazi kuwa mumeo anauwezo wa kwenda mwendo wa angalau Dk15-20 sio dakika  3  kama  ulivyosema!

Napenda utambue kuwa uwezo wa tendo kwa wanawaume unatofautiana kama ilivyo kwa baadhi ya wanawake, suala muhimu ni upendo mlionao (mnapendana) na yeye anauuwezo wa kulifanya tendo mpaka wote mnafikia mshindo nakuridhika.

Mawasiliano wakati wa Tendo:
Suala lingine hapa ni kutojua namna ya kucheza na wewe au mwili wako, kama unapenda kuchezewa zaidi kabla ya tendo la ndoa ni wajibu wako kuliweka hilo wazi na kumuelekeza mumeo wapi pa kushika, usitegemee yeye afanye hivyo kwani hajui nini unachokitaka au kukipenda. Ili ufurahie tendo na lifanywe your way unatakiwa kuwasiliana na mumeo wakati tendo linaendelea....


Kama nilivyosema hapo awali sio wanaume wote wanauwezo wa kufanya  mapenzi unaofanana, hivyo basi kama yeye anamudu asubuhi na jioni au asubuhi mchana na jioni (weekends) then kubali utaratibu huo kuliko kulazimisha afanye ulivyozoea wewe mara tatu katika saa moja.....ni ngumu kwa baadhi ya wanaume hasa wenye umri wa miaka 35 na zaidi.

Ni matumaini yangu utafanyia kazi ushauri kutoka kwa wachangiaji wengine na kuongezea maelezo ya hapo juu  ili kuishi maisha mazuri na yenye amani kwa faida yako, mumeo na watoto wenu

UFANYE NINI UKIGUNDUA PENZI LAKO LIMEINGILIWA NA MTU NA BADO UNAMPENDA ANAYEKUCHEAT?



Leo naomba tudiscuss topic hii,maana naamini kama sio wewe yanakukuta haya basi ndugu yako wa karibu au rafiki yako analalamikia hili...

Imewahi kutokea unampenda mtu sana na mmekaa kwa muda flani mrefuuuu,halafu katikati ya safari unakuja kugundua kuna kidudu-mtu,whether ni Mwanaume au Ni Mwanamke ameingia kwenye Penzi lenu na umekuwa Shareholder kwenye Kampuni ya Mahaba Limited???

Huwa unafanyaje ukigundua Mahabuba wako anaibiwa namtu flani na wewe bado unampenda???

Je unasusa na kuamua kumuachia Kidudu-mtu ashinde Battle kiulaini???

Au unakomaa na Battle na kumfunza adabu kidudumtu hadi anaachia ngazi???

Unatumia ujanja gani kama ni Boy wako na unampenda,lakii mchizi amefall kwa kidudu-mtu na unakaribia kutoswa na Mchizi kisa kanogewa na Penzi jipya tam tam???

Maswali ni mengi lakini all in all,LEO nataka nikupe Mbinu tu ambazo zitakufanya upigane hiyo vita na USHINDE....Ukifuata haya,Probability ya wewe kushinda na kutunza Penzi lako ni 0.7%...

Mambo haya ni muhimu uyajue maana yanatokea kila siku,Kama bado hayajakukuta basi yatatokea,Kula Shule,siku yakikukumba basi unajua Mlango wa kupigia Bao...TWENDE KAZI:

1.INAWEZEKANA KOSA NI LAKO

Mara nyingi tukiwa kwenye Mapenzi tunajisahau sanaaaaaa,tunahisi tumemaliza,nishampata basi inatosha..Ubunifu sifuri,we mbuzi kagoma tu miezi mia 7,hujui kitu ingine..Chalii angu inakula kwako...Mwenzio akitoka anapigwa Jackie chan,Mission Impossible 6 na Kandahar....We upoupo tu unaegesha kama Parking ya Corner Bar.....INAKULA KWAKO

Jambo la kwanza,weka possibility kwamba moja ya sababu zilizomfanya jamaa/demu atoke ni WEWE...Usi-throw lawama kwake tu wakati kumbe na wewe si ajabu ulikuwa na mapungufu yaliyochangia...

2.KUWA MPOLE

Ukishaweka Possibility ya wewe kuwa moja ya sababu we kuwa mpole...Jipange kwa mbinu za Comeback kama Manchester...Ukifungwa huendi nyuma kuanza kulia,unajipanga na mashambulizi ya kusawazisha..hiyo ndo Battle....

Sasa wengine wanapanic,wanaanza kumtusi jamaa/demu,ooh we malaya sana,umekosa nini kwangu.....ipo siku atakujibu,nakosa nyamaaaa,we unanipikia maharage tu!Utafanyaje???

Kupanic hakusaidii,tena ukipanic ndo atahamia kule mazimaaaaaaa,utabakia unatokwa povu tu mwenzio anapewa mijiraha!Kuwa Mpole

3.TAFUTA TATIZO NI NINI ILI UJUE UNAINGIA NA SILAHA GANI

Huwezi kuua Nzi na AK 47...Jua adui ni nini uchague Zana ya kudeal nae...

Hii ni mtihani pia kwa sababu kwa Mwanaume anayecheat kufunguka kwamba ni nini haswa kilichomtoa ni ngumu sana.....Na tatizo lingine ni kwamba hata akisema utamchukuliaje??Wanawake hawapendagi kuambiwa ukweli na ukimwambia,hata kama ndo ukweli atanuna mbaya,ufudu haingii!Mnuno haswa!Anauliza halafu ananuna.....Hilo moja,Wanaume nao ni worse...Akiuliza nini kimekutoa ukamwambia,ah we unanipa goma dakika 5 wakati mwenzio anasimamaia Show ya Fally Ipupa saa nzima...duh,mtu mzima unahisi umekosewa heshima unamwagia makofi!HAISAIDII!
Ukiambiwa we Selfish dakika 5 chali,chukua kama Positive issue na ujifunze...Kama huwezi zaidi ya dakika 5 jifunze wenzio wanasimamiaje kucha...Mwanaume dakika 5 aibu jamani khaaa,Mchuchu anapandisha Kilima anapishana na wewe ndo unaserereka kwenye ganda la ndizi.....Aaaaaaa,sio kiivyo!

Ukipata Kiini cha tatizo BADILIKA!Akisema unalewa sana humpi haki yake BADILIKA...Akisema humpigii simu na Mwasiliano yamekuwa hafifu na huku kwa Bi Kidude anapigiwa mara 76 kwa siku,BADILIKA.....Hakuna jinsi,kama Blunder ushafanya,wajanja wamefill GAP,Pigana ili arudi kwako kwa kubadilika kwa kile alichosema.

Kasheshe ni pale unapoambiwa tatizo ukakasirika....Au kutojibiwa kiini cha tatizo,,,Kila Ukiuliza anasema ah niliamua tu...au imetokea tu..Hapo unalo,inabidi utafute mahali muafaka pa kumuuliza,na most probably muda mzuri ni akiwa anakanyaga kitonga,hapo utajibiwa yote maana hisia zinakuwa ziko juu...

4.FANYA ANAYOPEWA KULE NA ZAIDI

Hakuna kitu kizuri kama kumpa Mpenzi wako vyote ili akose vya kuomba nje!

Usiache hata tundu moja la kidudu kuingia na kusambaratisha.....Mpe Mawasiliano kwa Asilimia Zote.....Mpe Attention....Mpe hela ukiweza...Mpe Mahaba makali yenye Kungfu,Taekwondo na Kila kitu....

Hakuna Mwanaume atamuiba maana unapata vyote....Hakuna Mwanamke atampa lolote ambalo wewe hujui,Viuno vyote wavijua,Feni Mbovu Style,Feni nzima,Air Condition Moves,Mupeeee.....

Kama umegundua tatizo ni Mahaba uliyokuwa unampa badilika,kuwa mbunifu from NOW going forward...Si unampenda???Usijali kwamba kuna Competition,wewe fanya kwa nafasi yako....Mchoshe hadi akiwaza kuamka kwenda kule akute hana nguvu tena,atabaki kwako..Dozi Tu!

Baada ya muda utagundua amerejea,Kule alikoibwa hakuna Jipya tena,atabakia wako na utaishinda vita ILA,Jifanye bandidu,eti unamnunia kwanini kaenda kule....Au unamtafuta huyo Mwanaume Mpya au Mwanamke Mpya unaanza kumtukana,eti ooh ntakukomesha,unaiba vya watu,mara ooh ntakuloga uvae chupi usoni...ah wapi,unafeli....Dawa ya mwizi ni kumkimbiza kimyakimya,wala kelele hupigi,mwenyewe atahisi huyu niliyemuibia leo sio wa kawaida,ila makelele ya mwizi mara vile,wote mtaonekana wezi.....

PIGO : PAROKO WA RC IFUNDA APOTEZA MAISHA KATIKA AJALI AKITOKA MSIBANI NJOMBE




     Hili ndilo gari ambalo  limesababisha  kifo cha paroko
             -------
PAROKO  wa kanisa la RC parokia ya Ifunda Alphonce Mhamilawa amefariki  dunia katika ajali mbaya ya gari  iliyotokea katika eneo la Sabasaba Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Mashuhuda  wa  ajali  hiyo wameueleza mtandao  huu  kuwa ajali  hiyo ilitokea  majira ya saa 2 usiku  wa  kuamkia  leo wakati paroko  huyu akitoka mkoani Njombe katika  shughuli  ya Mazishi

Mmoja kati ya mashuhuda  hao Bw  Saugo Ndemo  alisema  kuwa paroko  huyo alikuwa akiendesha gari dogo aina ya Toyota  Hilux (Pick Up) yenye  namba  za usajili  T434 APP mali ya Kanisa la Roman Katoliki Parokia ya Ifunda.

Ndemo  alisema  kuwa chanzo  cha ajali  hiyo ni Paroko  kuligonga gari aina ya Lori  kwa  nyuma na kuwa lori  hilo halikuweza  kusimama.

Alisema  kuwa  paroko  huyo alifia eneo la tukio baada ya  ajali  hiyo  iliyopelekea  kichwa  chake  kupasuka.

Mmoja kati ya askari  wa usalama barabarani ambae hakutaka  kutaja jina lake kwa  kuwa si msemaji  mkuu  wa  jeshi la  polisi alisema  kuwa  chanzo cha ajali  hiyo ni mwendo kasi.

Pia alisema kuwa lori ambalo paroko huyo aliligonga linasadikika  kuwa lilibeba mbao huku  likivutana na  lori  jingine na baada ya ajali  hiyo halikuweza  kusimama.

MSANII SIZE NANE ANAILILIA BIKRA YAKE HADHARANI





Mwanamuziki  aliyeitikisa vilivyo Kenya kabla ya kuokoka na kuachana na muziki wa kidunia, mwanadada Size 8 sasa ameanza kufunguka katika interview kwenye vituo mbali mbali vya redio na Tv kuhusiana na maisha mapya ya kidini.

Kati ya  mambo yote ambayo Size 8 amekuwa akiyaongelea, ni moja tu ambalo amekuwa akilitilia mkazo kwa kumaanisha kuwa linamsikitisha zaidi .....Jambo hilo ni lile la kupoteza BIKRAYAKE.....
Size 8 ameziambia media kuwa  "Najutia sana kupoteza bikra yangu. Ninaamini kuwa kijana anatakiwa kujilinda na kujizuia kufanya ngono katika ujana wake wote mpaka atakapo pata kibali toka kwa Mungu."

DAYNA NYANGE AMPIGIA SALUTI AFANDE SELE KWA TUNGO KALI





Mwanamuziki  toka  mkoani  Morogoro  anayefanya  poa  kwa  sasa  na  wimbo  wake  wa  Leo  mwanadada  Dayna  Nyange  a.k.a  Mkali  wao,  amefunguka  na  kumpigia  saluti mwanamuziki  mkongwe toka  hapa  Morogoro Afande  Sele.

Akiongea  na  mwandishi wetu   toka jijini Mwanza  aliko  sasa  katika  ziara  ya kimuziki  na  uzinduzi  wa  Albam  ya  Kala.  Dayna  amesema  huwa  anamkubali  afande kwa  tungo  zake

 '' kwa  kweli  siku  zote,  nimekuwa  nikimkubali  sana  Afande  sele  kwa  tungo  zake  zenye  ujumbe,  lakini  kwa  wimbo  huu wa  Dini tumeletewa,  nampigia  saluti.
 Afande  ni  bonge  la msanii  na  huwa naskiliza  nyimbo  zake kwani  najuwa  nikiskiliza  nyimbo  zake  kuna  madini  napata,  lakini  sasa kaka  mkubwa  kwa  hapa  alipofikia  na kufikilia  kwa  kina juu  ya  wimbo  huu,  anastahili  kuwa mfalme wa  Rhyme,  waliompa  tuzo  hawakukosea. 

Big  up  sana  Afande, saluti  kwake,  aendelee kuwa  mwalimu  wa  ujumbe  , huuwimbo  ni  zaidi  ya  Hotuba  ya  kitaifa Inayotolewa  na  Rais'' Amesema Dayna
 Ubalozini

"SIONI TATIZO KWA LULU MICHAEL KUPIGA PICHA NA PENNY....HUO NI UMBEA WA MAGAZETI"..WEMA SEPETU




Hivi  karibuni  zilisambaa  picha  za  Lulu  Michael  akiwa  katika  picha  ya  pamoja  na  Penny....

Picha  hizo  zilizua  utata  mkubwa  miongoni  mwa  watu  huku  kundi  kubwa  likidai  kuwa  picha  hizo  zimepigwa  makusudi  kwa  lengo  la  kumuumiza  Wema  Sepetu...
 Lulu Michael  akiwa  na Penny

Madai  hayo  yaliandikwa  kwa  kina  na  gazeti  moja  la  udaku  hapa  nchini  likisimulia  ugomvi   uliopo  kati  ya Penny  na Wema Sepetu.....

Waswahili  husema:
             Kama  A=B   na    B=C    basi   C= A  pia...!!!! 

Huo  ndo  ulikuwa  mtazamo  wa  gazeti  hilo  kusuhu  ukaribu  wa  Penny  na Lulu Michael.....

Akizijibu  tuhuma  hizo,Wema  Sepetu  ameamua  kuvunja  ukimya  na  kudai  kuwa  hawezi  kuwa  na  beef  na  baby  wake  Lulu  kwa  sababu  ya  Penny.....

"UREMBO SIYO KIPAJI NA SI KILA MWANAMKE MZURI ANAWEZA KUIGIZA"...JACKLINE WOLPER




Muigizaji Jacqueline “Jackie” Wolper amewashangaa wanaodhani kuwa urembo wa mwanamke ni mbadala wa kipaji hasa katika sanaa ya maigizo. 


Alisema urembo ni moja ya sifa ya mwanamke lakini kamwe hauwezi kumfanya asiye na kipaji kuwa nacho.
  
“Ukiwa mrembo ni bora zaidi,kwa kuwa itamfanya avutie kwenye movie,lakini pamoja na hayo ni lazima awe na uwezo wa kuigiza kulingana na kipande husika”alisema Wolper.
  
Wolper aliendelea kulalama kuwa kila mtu akijona ana sura ya kuvutia na umbo zuri basi anajua anaweza kuigiza ndio maana matokeo yake wanafanya vitu sivyo na mwisho wake wanaacha fani kabisa.
  
Alifafanuwa kuwa kuigiza ni zaidi ya urembo hivyo yeyote ambaye anafikiri anaweza kufanya kazi hii kwa uzuri wa sura na umbo ajaribu kama hakuchemka.

Source: Mwananchi

"SIWAOGOPI MATAIRA WANAONIPONDA....MUNGU PEKEE ANAWEZA NA SI HAO TUMBIRI".....HII NI KAULI YA DIAMOND





Watu kadhaa  wamekuwa  wakimponda Diamond  baada ya  kwenda LONDONI kwa  madai kuwa ni mshamba  wa  jiji  na  limbukeni ....

Madai hayo yamekuja  baada ya msanii huyu kuanza kuyashobokea  magari ya kifahari kwa kupiga nayo  picha na kuzirusha hewani.....

Baada ya kuona  mizengwe  ya watu imekuwa  mingi, Diamond  ameamua kuwajibu  kwa kupost  jumbe  huu