Nassari pamoja na mambo mengine amemtembelea Lema ili kujua kilichotokea wakati akizungumza na wanafunzi wa Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA) na baadaye kukamatwa na polisi.
Mbunge huyo Arumeru Mashariki amewasili Leo Arusha na kwenda moja kwa moja katika Kituo Kikubwa Cha Polisi (Central).
Jana Nassari alinukuliwa akisema kwamba Leo yeye na Halima Mdee (Kawe) watakutana na kuzumgumza na Mulongo kuhusu
kilichotokea katika chuo hicho cha uhasibu na kusababisha kukamatwa kwa Lema.
“Jumatatu (leo) tunatarahia kuonana na mkuu wa mkoa na tayari nimempa taarifa. Tunataka kuzungumza naye kilichotokea na hali ya kisiasa iliopo Arusha hivi sasa,” alisema Nassari.
Mpaka sasa haijafahamika Nassari amezungumza nini na Lema.
No comments:
Post a Comment