Sunday, March 31, 2013

KIJANA AAMUA KUCHOMA MOTO KITAMBULISHO CHA TAIFA CHA KENYA MARA BAADA MAHAKAMA KUHALALISHA USHINDI WA KENYATTA HAPO JANA




Kijana ROBERT STEPHENE OKELLO mwenye asili ya Luo ameingia matatani mara baada ya kuamua kuchoma kitambulisho chake cha Utaifa mara baaada ya mahakama kutengua Pingamizi la Mgombea kupitia Tiketi ya  ODM bwana RAILA ODINGA kupinga Uchaguzi huo.

Kijana huyo aliamua kufanya hivyo kutokana na kile alichokiita kuwa ni Uonevu wa kisiasa na hivyo kupelekea kukichoma kitambulisho hicho ambacho kikatiba ni mali ya Jamhuri ya watu wa Kenya.

Hata hivyo Mahakama Nchini humo haijazungumza kitu chochote mpaka sasa na kuna wasi wasi mkubwa kuwa huenda pakatokea hali ya hatari zaidi kama mahakama itachukua Uamuzi wa kumtia mbaroni kiajana huyo

No comments:

Post a Comment