Monday, May 13, 2013

"MAKALIO YA LOVENESS DIVA NI MACHAFU.....KWANZA MTU MWENYEWE NI NJITI"...HAYA NI MATUSI TOKA KENYA BAADA YA DIVA KUPARAMIA PENZI LA PREZZO



Vita  kali  ya  matusi  ya  nguoni  imeibuka  kati  ya  Loveness Diva  wa Bongo na Lady Boss  wa  Kenya  kisa  kikiwa  na  PENZI  LA  PREZZO..... 

Mwanadada maarufu nchini Kenya  maarufu  kwa   jina  la  Huddah Monroe leo  ameingia  kwenye  bifu  kali  na   Tanzanian Diva, Loveness Love, kwa  madai  kwamba  Diva  ameparamia  penzi  la  mpenzi  wake  ambaye  ni  prezzo....
  
Mrembo  huyu  anashangaa  kuingiliwa  penzi  lake  na  mtu  kama  Diva....Kwa  upande  wake  anamchukulia  Diva  kama  mwanamke  mchafu, Njiti,asiye  na  makalio ya  kuvutia  na  kahaba......

Naomba  nisiyamalizie  matusi  yao.....Hizi  ndo  tweets  za  huyo  mrembo  wa  kenya...  











LADY JAYDEE KURIPOTI MAHAKAMANI Leo


MWANAMUZIKI nyota wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ kesho (Jumatatu) anatarajia kuripoti Mahakama ya Kinondoni  kufuatia taarifa alizofikishiwa Meneja na mume wa msanii huyo, Gadna G Habash ‘Captain’.
Gadna alisema ni kweli wamepata taarifa za kutaarifiwa Lady Jaydee kufika Mahakama ya Kinondoni, kesho (Jumatatu) Mei 13, mwaka huu.
 

“Ni kweli tumepata wito na Mahakama ya Kinondoni, hii ni baada ya kufika watu ambao walijielezea kuwa wanatoka Mahakama hiyo jana na kuleta barua ya kumkabidhi Lady Jaydee mwenyewe japo hawakumkuta” alisema Gadna. 


Katika ukurasa wa Twitter wa Lady Jaydee saa tatu zilizopita aliandika hivi "Sumu ya teja Ukonga, Keko, Segerea. Kesho Mahakamani kizibiti ubaoniii eeeh aaah!" wakati siku ya Ijumaa katika ukurasa wake wa Facebook aliandika hivi: 


"Ratiba ya usiku wa leo ni MACHOZI BAND kama kawaida, ila ratiba ya Jumatatu natakiwa Mahakama ya Kinondoni... Taarifa zaidi zitafuata nikijua kinachoendelea... Ila kwa leo mje tuburudike Nyumbani Lounge mpk asubuhi."

MFANYABIASHARA ALIYEFUMANIWA NA MWANAFUNZI GESTI APIGWA FAINI YA 640,000




YULE mfanyabiashara  wa jijini Dar ambaye hivi karibuni alifumaniwa gesti akiwa na mwanafunzi wa kidato cha pili, huenda akapandishwa kizimbani siku yoyote.....

Kwa mujibu wa dada wa mwanafunzi huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe , baada ya mfanyabiashara huyo kufumaniwa na binti huyo mwenye umri wa miaka 16, aliahidi kutoa fedha za Kimarekani dola 400 (zaidi ya Sh. 640,000) kama faini kwa kitendo hicho.

Hata hivyo, pamoja na kukubali kutoa kiasi hicho, mfanyabishara huyo hakutimiza ahadi yake na kuamua kuingia mitini.
 

Dada wa mwanafunzi huyo amedai  kuwa   mfanyabiashara huyo anasakwa ili wamburuze mahakamani kutokana na mwisho wa mwezi uliopita kushindwa kutimiza ahadi yake.
 

“Aliandika kwa mkono wake kwamba atamlipa huyu mwanafunzi fedha hizo kama fidia ili akalipie ada ya kuendelea na masomo, lakini mpaka leo hii hajaonekana na wala simu yake ya mkononi haipatikani, tukimkamata tutamburuza mahakamani kwa sababu sheria hapa Bongo hazifuatwi kabisa kwani tulitarajia vyombo husika vingeingilia kati lakini hakuna lolote,” alisema dada huyo.

Aidha, dada huyo alisema kuwa wanatarajia kwenda kuchukua hati ya kumkamata mfanyabiashara huyo ‘RB’ katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar ili waweze kumsaka.



“Ushahidi tunao tena wa uhakika kabisa, kaandika kwenye karatasi na katia saini yake, tena mwandishi naomba na zile picha alizopigwa akiwa chumbani na mdogo wangu ili zinisaidie katika ushahidi wa mahakamani,” alisema dada huyo huku akionesha karatasi ambayo waliingia makubaliano ya kulipwa dola hizo 400 na mfanyabiashara huyo.
Jumatano ya Aprili 24, mwaka huu mfanyabiashara huyo alifumaniwa na denti huyo katika chumba namba 107 ndani ya gesti moja iliyopo Kinondoni, Dar 

"AKINA DADA ACHENI KUJICHUBUA....NJOONI NIWAPE MBEGU ZANGU ZA KIUME ZIWANG'ARISHE"....HII NI KAULI YA MBUGE KESSYY




MBUNGE wa Nkasi Kaskazini, Ally Kessy (CCM) alhamisi  ya  wiki  hii  aliwavunja mbavu wabunge baada ya kuwasuta wabunge wanaojichubua ngozi akiwaambia wanaohitaji ngozi nyeupe wamuone.



Ameitaka pia Serikali isiishie kukamata waingizaji wa vipodozi hatari, bali pia watumiaji wakiwemo wabunge. Kessy alisema Serikali inapaswa ikamate na watumiaji wa vipodozi hivyo kama ambavyo huwa inafanya kwa waingizaji na watumiaji wa dawa za kulevya.


Akichangia wakati wa kujadili vifungu kabla ya kupitisha bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii juzi, alisema inashangaza kuona katika meza za kujipodoa za wanawake wakiwemo wabunge, vimejaa vipodozi lakini serikali haiendi kuwakamata.


Alisema hata bungeni wapo wanawake wanaotumia dawa za kubadilisha sura kiasi kwamba wakienda vijijini kwao, ndugu zao wanawakimbia, lakini Serikali haiwakamati.



“Wanajiharibu sura huwezi kujua ni raia wa nchi gani; unashindwa kujua hawa ni Wachina, Wajapani ukianzia humu humu bungeni,” alisema Kessy na kusababisha kicheko bungeni.

Mbunge huyo aliendelea kuwavunja mbavu pale ambapo alisema wanaotaka kubadilisha rangi zao, wawaone watu weupe kama yeye wawape mbegu.


Kessy alitoa utani huo baada ya Naibu Spika, Job Ndugai kumtania akisema “Na wewe ni matokeo ya vipodozi hivyo,” akimaanisha weupe wa Mbunge huyo.

“Nashauri wanaotaka kubadilisha rangi zao watuone sisi tuwape mbegu,” alisema na kuendelea kusababisha ukumbi mzima wa bunge ulipuke kwa kicheko.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi alisema jukumu la wizara yake ni kuangalia usalama wa vipodozi na haijihusishi kujua nani anatumia na nani hatumii.


Alisema wajibu wake ni kuhakikisha vipodozi vinavyoingia nchini vinakuwa na viwango. Alisema wanaotumia ni hiari yao kwa kuwa Wizara ikiingilia, utakuwa ni ubaguzi wa kijinsia.


Hata hivyo, Dk Mwinyi alisema watumiaji wanapaswa kuhakikisha kwamba vipodozi husika vimethibitishwa usalama wake.

"NATAFUTA MWANAUME WA KUNIZALISHA...." AISHA BUI WA BONGO MOVIE




Baada ya kuadimika kwa muda mrefu, mwigizaji wa filamu za Kibongo, Aisha Bui ameibuka na kusema kuwa anatafuta mwanaume ambaye atamzalia mtoto na hatimaye waoane ila akadai wa kumuoa kwa sasa hamuoni.


Akizungumza na mwandishi wetu,  Aisha amefunguka kuwa alikuwa kimya kwa sababu kuna mambo alikuwa akifanya.
Alisema kwa kuwa ameyakamilisha, sasa ana nafasi ya kusaka mtoto iwapo atampata mwanaume sahihi.

Aisha amevitaja vigezo vya mwanaume wa kumzalia kuwa amjengee nyumba ya kuishi yeye na mtoto wake kisha awe na uwezo wa kumlea na kumpatia elimu bora.

MTOTO WA MIEZI MIWILI ANAJISIWA...




Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vimeendelea kutokea nchini licha ya kupigwa vita kwa kampeni mbalimbali

Baadhi ya ukatili huo ni pamoja na kubakwa na ule wa kukatwa viungo vya mwili kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino).
 

Licha ya kupigiwa kelele, hata kampeni mbalimbali za kupinga kufanyika, unyama huo umeendelea kufanyika na tukio la hivi karibuni limemhusisha mtoto Erisia Tito mwenye miezi miwili anayedaiwa kunajisiwa wilayani Mpwapwa Mkoa wa Dodoma.
 

Tukio hilo limekuwa gumzo katika mitaa mbalimbali wilayani humo, huku baadhi ya wananchi wakidai kuwa linahusiana na imani za kishirikina.
 

Unaweza kujiuliza maswali mengi, hata inakuwaje mtoto wa miezi miwili kunajisiwa?
 
 

Katika vijiwe vya kahawa wilayani Mpwapwa, hii ni habari kubwa zilizokuwa zikizungumzwa kuhusu kunajisiwa kwa mtoto huyo swali likibaki; Je, yule mtu alimnajisi mtoto ameishia wapi?

Naingia chumba cha Mganga Mkuu Wilaya ya Mpwapwa kupata maelezo ya mtoto huyo tangu alipofikishwa katika hospitali ya wilaya hiyo, maendeleo yaliyofikiwa na utaratibu wa kiuchunguzi unavyoendelea.
 

Kauli ya Mganga Mkuu
 
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, Lunemo Sakafu anasema kuwa tangu alipolazwa, mtoto huyo alikuwa akipelekwa kliniki kwa ajili ya kupatiwa chanzo mbalimbali na kupima afya yake, kwamba alikuwa na afya nzuri.

“Hakuzaliwa katika hospitali hii ila alikuwa akihudhuria kliniki, alizaliwa kwa wakunga wa jadi na mara ya mwisho kuja hapa hospitali ilikuwa Aprili 15, mwaka huu na alikuwa na afya nzuri,” alisema
 

Ashangazwa
 
Alisema kuwa alishangazwa na hali aliyokuwa nayo mtoto huyo alipofikishwa kwa mara nyingine katika hospitali hiyo kwani alikuwa akitokwa haja zote bila kikomo.

“Tunampatia matibabu ya kina ili kujua tatizo ni nini. Kwa sasa tuna utaratibu wa kumpeleka katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma ili akafanyiwe vipimo vya kina kwa kuwa mtoto huyu anatoa haja zote bila kikomo,” anasema Sakafu.
 

Sakafu anasema hata wazazi wa mtoto huyo walipoulizwa juu ya hali aliyonayo mtoto wao, walipishana kauli katika maelezo yao na kwamba jambo hilo liliwatia shaka.
 

Kauli za wazazi
 
Baba wa mtoto huyo, Silvani Msemakweli anasema kuwa tangu mtoto wake alipozaliwa alikuwa na maumivu wakati wa kupata haja kubwa.

“Tangu alipozaliwa hali hii ilikuwapo hasa wakati wa kujisaidia haja kubwa mtoto analia, kwani husikia maumivu makali. Katika ukoo wetu yupo mmoja wa ndugu zetu aliyewahi kuwa na mtoto aliyekumbwa na hali kama hii ya mtoto wangu,” anasema na kuongeza:
 

“Yeye alipona baada ya kutumia dawa za kienyeji na alipona kabisa, siyo kweli kuwa mtoto alinajisiwa.”
 

Msemakweli anaongeza kuwa ni vigumu kuamini kama mtoto huyo amenajisiwa kutokana na mazingira ya familia hizo mbili, yaani familia yake na ya mke wake.
 

“Japo sikuwapo siku hiyo, lakini bado siamini kama mtoto wangu atakuwa amenajisiwa. Kwa sasa mama yangu ndiyo anayeshikiliwa na polisi na kufunguliwa kesi,” anasema Msemakweli.
 

Mama wa mtoto huyo, Rejina Msemakweli anasema kuwa yeye alijifungua kwa mkunga wa jadi aliyemtaja kwa jina la Hilda Maderemo na kwamba mtoto alikuwa mzima na hakuwa na tatizo lolote.
 

Anasema kuwa baada ya kujifungua alianza kumpeleka mtoto huyo katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa kwa ajili ya kupata chanjo mbalimbali.
 

“Mwanangu nilimzaa akiwa mzima nilishangaa siku moja analia sana wakati huo alikuwa amepakatwa na bibi yake,” anasema na anaongeza:
 

“Nilimwacha na bibi yake kwa kuwa nilikwenda shambani ila niliporudi nilimkuta akiwa analia kupita kiasi. Nilimchukua na kumwogesha, lakini kabla sijamaliza niligundua kuwa ameumia sehemu zake za siri na alikuwa akitoka kinyesi mfululizo, yaani mbele na nyuma.”
 

Regina anaeleza kuwa familia yake ina watoto wawili ambao wote ni wasichana, mume wake pamoja na mdogo wake wa kike, kwamba pia wanaishi kwa ukaribu mkubwa na familia ya mume wake.
 

“Katika maisha yetu nimekuwa nikiishi na wakwe zangu bila maelewano mazuri, familia imekuwa ni yenye kugombana kila wakati, hata kama kitu ni kidogo. Lakini yataibuka mambo makubwa kiasi kwamba utadhani ni watu wasio familia moja inaniuma sana,” alisikitisha.
 

“Naongea kwa kuvumilia tu, lakini moyoni ninaumia kwa kiasi kikubwa kuona mwanangu amekuwa katika hali kama hii sielewi. Tukijaribu kumwuliza mama mkwe wangu hasemi ukweli kuwa mtoto amekuwaje,” anasimulia Regina huku akilia machozi.
 

Anasema kuwa aligundua kwamba sehemu za siri za mtoto wake zimevimba na kuonyesha kukwaruzika huku akitokwa na kinyesi bila kikomo.
 

Kauli ya mkunga
 
Mkunga Hilda Mademo anakiri kuwa alimzalisha Regina na kwamba mtoto huyo alikuwa mzima bila kuwa na kasoro yoyote.

“Mimi ndiye niliyemzalisha mama huyo na mtoto alizaliwa akiwa mzima kabisa. Suala la kupatikana kwa tatizo hilo, ukweli wanao wazazi wenyewe. Huduma zangu nilizitoa hata hospitali ya wilaya inalifahamu, walinitembelea hadi hapa kuona mazingira ninayofanyia kazi na kunisaidia baadhi ya vifaa kwa mfano haya mabakuli,” anasema Hilda.
 

Polisi yatoa tamko
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Polisi David Misime anakiri kupokea taarifa za kunajisiwa kwa mtoto wa miezi miwili katika Kijiji cha Ising’u wilayani Mpwapwa.

“Sisi tulipokea taarifa hiyo na kuanza kuifanyia kazi za awali, hadi sasa bibi wa mtoto huyo yuko mikononi mwa polisi. Tunasubiri jibu la kitaalamu kutoka kwa daktari kwa kuwa wakati mtoto amepelekwa katika hospitali,”alisema Misime na kuongeza:
 


“Katika Kituo cha Polisi hapakuwa na ushahidi wa kujitosheleza kwa kuwa mtoto huyo tayari alikwishasafishwa siku tatu zilizopita.”

Viongozi wa Serikali wakemea
 
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mkoa wa Dodoma, Ryoba Kangoye amekemea vikali tukio hilo na kuliita ni la ugaidi kwa kuwa mtu huyo hakuwa na nia ya kubaka bali ni kuua.

“Hii hali siyo ya kawaida ni mstuko mkubwa kusikia hili kama hiyo kujitokeza katika mazingira hayo. Hivi, Mtanzania wa leo kufikia kufanya jambo kama hilo ni ajabu kubwa, hata hiyo familia kukaa kimya ni kunyima haki vyombo vya sheria kufanya kazi zake na kupoteza ushahidi uliokamika,“ anasema Kangoye.
 

Mtendaji wa kijiji hicho, Emmanuel Mamba anasema kuwa waliposikia tukio hilo walijikuta ni kama wamemwagiwa maji au tindikali wakilifananisha na mauaji.
 

“Tulioposikia tuliishiwa na nguvu kwa kuwa hata kama matendo kama hayo hufanyika, basi isingekuwa kwa mtoto mdogo kama huyo, asiye na uwezo wowote ule. Tulijiuliza maswali mengi hata kuhisi huenda walitaka kumfanyia ukeketaji,” anasema Mamba
 

Viongozi wa dini
 
Kwa niaba ya madhebu ya dini, Padiri Masasi Deo kutoka Kanisa la Katoliki Mpwapwa, amekemea vikali tabia hiyo akisema:

“Nionavyo sasa umefika wakati wa watu wenye dhamana na jamii kukaa pamoja na kufanya ibada na kujua mbinu mpya ya kufundisha maadili kutokana na hali ya maadili ilivyobadilika nchini.”
 

Haki za binadamu
 
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu (AFNET)Mkoa wa Dodoma, Sara Mwanga amesema kuwa kitendo hiko ni unyama na kwamba jamii bado haina elimu ya kujitambua kuhusu ukatili unaofanywa hasa katika kushughulikia kesi za aina hiyo.

“Watoto wengi wamekuwa wakiumizwa, lakini mwishowe hakuna linalofanyika katika kumtetea mtoto huyo kutokana na wahalifu huachiwa huru kwa kile kinachodaiwa ushahidi haujakamilika. Kwa kweli kuna utata mkubwa katika suala hilo,” alisisitiza.
 

Aliitaka Serikali kupitia vyombo vya dola kuwa makini katika kuangalia namna ya kupatikana kwa ushahidi ili kutenda haki kwa watoto wanapoumizwa, badala ya watuhumiwa kuachiwa huru kwa madai kuwa ushahidi haujakamilika.
 

HAYA NDO MAJINA 11 YA WAREMBO WALIONASWA WAKIFANYA MAPENZI NA MBWA HUKO MOMBASA




Sakata  la  warembo  11  wa Mombasa  kunaswa  wakiiigiza  video ya ngono  na MBWA  limechukua  sura  mpya  baada  ya  taarifa  kuvuja  kwamba  yule  mzungu (Christopher Clement) waliyekuwa  naye  ni  mfanyakazi  wa  shirika  la umoja  wa mataifa ( United Nations Development Programme -UNDP)

Madai  hayo  yamekuja  baada  ya  kunaswa  kwa  gari  mojawapo  la  mzungu  huyo  lenye  namba  za  usajili  40UN221K  ambazo  ni  za  UNDP....

Na  haya  ndo  majina  11  ya  watuhumiwa  wa  kashfa  hiyo  chafu.....
  1. Christopher Clement Weisssenrieder, 
  2. Janet Akoth Omollo, 
  3. Mercy Waithera Karanja, 
  4. Mary Nyambura Kimani, 
  5. Magdaline Wairimu Chege, 
  6. Celestine Nekesa Sitati 
  7. Dorcus Melishah Indakwa
  8. Lydia Nyaboke Momanyi, 
  9. Philidelia Mawia Solomon, 
  10. Anne Wanjiku Gichuki 
  11. Celilia Nzambi Katuku.

Sunday, May 12, 2013

MAMA AMCHOMA MOTO MTOTO WA WIFI YAKE SEHEMU ZA SIRI KWA KOSA LA KUNYWA UJI WA MTOTO




ELIZABETH Bureko (26), mkazi wa Kata ya Nyamatare, Manispaa ya Musoma, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Musoma, kwa tuhuma za kumchoma na moto sehemu za siri mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minane.
 


Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Baraka Maganga, ilidaiwa na Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Sajini Stephano Mgaya, kuwa mwanamke huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 24 mwaka huu, saa 3 asubuhi.

Kwa mujibu wa mwendesha mashitaka huyo, mshitakiwa alikiuka kifungu cha sheria namba 169 cha mwenendo wa makosa ya jinai kama sheria hiyo ilivyofanyiwa marekebisho na kuwa namba 16, mwaka 2002.

Alidai kwamba, mshitakiwa huyo alimchoma katika sehemu zake za siri na mdomoni baada ya kumtuhumu mtoto huyo wa wifi yake, kwamba alikuwa akinywa uji wa mtoto aliyekuwa akimnywesha.
Mshitakiwa alikana shitaka na kurudishwa mahabusu hadi Mei 25 mwaka huu, kesi yake itakapotajwa tena

NGONO ZEMBE ILIVYOKITHIRI BARABARA YA KUELEKEA ZAMBIA



 makahaba-ngono-zembe

Licha ya kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya Ukimwi, Mkoa wa Mbeya bado unatajwa kuwa eneo lililokithiri kwa vitendo vya ngono bila kuwa na tahadhari (ngono zembe).

Sababu kubwa ya hali hiyo inaelezwa kuwa ni kuwepo kwa maegesho ya malori ya mizigo yanayoelekea Zambia huku madereva wake wakitajwa kuwa wateja wakubwa wa ngono.


Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi  katika maeneo yanayotajwa kwa biashara ya ngono yaani Kata ya Igawa na Igurusi, umethibitisha kuwepo kwa vitendo hivyo.  

Igawa
Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa madereva wa taxi eneo la Igawa aliyejitambulisha kwa jina la Felix, alisema kuwa kwa sasa biashara hiyo imedorora kwa sababu madereva wa malori wamepunguza kusimama hapo.  


“Zamani ungefika hapa saa hizi ungewakuta barabarani kabisa. Lakini siku hizi, malori yameacha kusimama hapa, ndiyo maana nao wamepungua. Lakini wapo baadhi yao ni wahudumu wa baa,” alisema dereva huyo.

Kwa kuwa muda ulikuwa umekwenda na usafiri usiku ni wa shida, mwandishi aliendelea Kata ya Igurusi kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Igurusi

Ni majira ya saa mbili usiku, baada ya kuchukua chumba kwenye nyumba ya wageni iliyo mbali na barabara kuu, nikarudi kwenye baa moja. Kabla sijaondoka, nikamuuliza mama mwenye gesti kama naweza kuleta mwanamke wa kulala naye. Akanijibu kuwa ni uamuzi wangu kwani haizuiwi.

Nilipofika katika baa moja iliyo pembeni mwa barabara (jina linahifadhiwa) nilikuwa nikipata kinywaji huku nikiangalia jinsi ya kumpata mtu wa kuzungumza naye kwa kina.
Namjaribu mhudumu mmoja wa baa hiyo kwa kumtongoza, lakini akasema hawezi kutoka na mimi kwa kuwa bado yuko kazini.


Nahamia baa nyingine ng’ambo ya barabara kwa lengo hilohilo. Hapo nakutana na mama mmoja wa makamo, kisha kumweleza shida yangu kwamba natafuta mwanamke wa kulala naye usiku huo.

“Ni kweli hapa wapo kina dada, ukiwataka mnaelewana tu. Mimi mwenyewe ninaye binti yangu ila nimetuma dukani, labda umsubiri. Lakini kama unaona utachelewa, basi nenda baa ya jirani hapo wapo wengi tu,” alisema mama huyo.

Nikaamua kwenda kwenye baa hiyo jirani na hapo nawakuta kina dada wapatao watano, huku wateja wakiwa wachache tu. Nikaagiza soda na kuanza kuinywa taratibu. 


Bila kupoteza muda nikamuuliza dada aliyeniletea soda (jina linahifadhiwa)  kama naweza kupata mshichana wa kulala naye usiku huo. Mahojiano yetu yakawa hivi
 

Mhudumu: Hapa wapo wengi tu… wote unaowaona hapa ndiyo kazi zao, sijui unamtaka nani?
Mwandishi: Mimi nakutaka wewe..

Saturday, May 11, 2013

" HAKUNA KANISA LILILOSHAMBULIWA KWA BOMU JIJINI DAR LEO "...HII NI KAULI YA KAMANDA KOVA




Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kova amesema Taarifa zilizoenea kwamba Bomu limelipuka katika Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT), Kunduchi jijini Dar es Salaam zimeenea ndivyo sivyo na kwamba askari walikuwa wanapambana na majambazi.

Wakati taarifa zikiwa zimesambaa katika mitandao ya kijamii na mitaani kwamba kuna kanisa la KKKT limeshambuliwa na bomu hivi punde, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kova amesema kwamba taarifa hizo sio za kweli na kwamba askari wa jeshi la polisi walikuwa wanapambana na majambazi karibu na eneo la kanisa hilo. 


Katika mapambano hayo polisi waliwarushia majambazi hayo bomu ili kuyakamata.

"Wakati askari wetu wanapambana na majambazi hayo- waumini wa kanisa hilo wamejitokeza kuwasaidia askari wetu. Naomba unisaidie kukanusha siyo kweli, nitazungumza na vyombo vingine vya habari kuweka sawa," amesema Kamanda Kova hivi Punde. 

MIKE TEE, PROFESA JAY, JAY MOE NA JUMA NATURE WATUMIA VIFARU VYA KI VITA KTK KUSHOOT VIDEO YAO?





Wasanii wakongwe wa Bongo Flava kutoka kushoto waliovaa kiraia ni Jay mo, mike tee, Juma Nature na profesa Jay wakiwa na wanajeshi
Picha hizi unazoziona ni post ya facebook ya Rapper and CEO wa kampuni ya Show BIZ Mike Tee Mnyalu na amezipost jana na kuandika  namnukuu "Wanaume Kazini Today tumeanza kushoot video yetu mpya soon tittle ntawajulisha its Under ShowBiz Defined Media" Swali je story line ya video hiyo itakuaje kuaje?
punguza kiraru raru, tusubiri tyme itafika.....
Mike Tee, Jay Moe , Profesa Jay na Juma Nature

YOU HEARD : PREZOO NA DIVA LOVENESS LOVE WAPO KWENYE MAPENZI MOTO MOTO




PREZZO
                                                                   IN LOVE WITH
DIVA LOVENESS LOVE
 Taarifa za siri ambazo zimefika mezani kwa muhariri zina nong'oneza kwamba Rapper tajiri nchini Kenya kwa sasa hivi yuko katika mahaba mazito na Mtangazaji wa kituo cha radio kikubwa nchini Tanzania, namzungumzia Diva Loveness Love wa Ala za Roho, inasemekana mahusiano yao yalianza wiki za karibuni baada ya Prezoo kudondoka bongo na alialikwa kwenye kipindi cha Ala za roho ndipo picha zima lilipo anzia, kama utani wakaanza kutania taniana, sasa usiku wa tukio hawakufanikiwa kwenda out lakini namba zilibadilishwa pale, kilichofata baada ya hapo sasa Prezzo akataka kwenda mpaka kwa kina binti lakini akazuiliwa wataalamu wa mambo wanasema penye nia pana njia, basi huenda time navyozungumza japo Prezzo hayuko bongo narudia tena huenda mambo yao yako bam bam kwa njia ya simu.
Muhariri alipojaribu kucheki na Diva, mwanadada akapangua shuti kuleeeeee, na kudai kuwa yuko na boyfriend wake wa kitanzania na PREZZO ni mshkaji tu.
alipovutiwa wire PREZZO jamaa akajaa mzima mzimaaaa, na kutiririka ya moyoni kuwa ni kweli anampenda Diva na mipango mengine inafata.
Skiza YOU HEARD HAPO CHINI:

VIGOGO WA DUBAI WAMGOMBANIA LULU MICHAEL ....




HABARI zilizonaswa na mwandishi  wetu  zinaeleza kuwa nyota wa sinema Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameitwa katika Jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kwa ajili ya kula  bata ikiwa ni pole yake kwa kusota Gereza la Segerea kwa karibu mwaka mmoja.

Chanzo kimoja  kilipenyeza habari kuwa mapedeshee hao wamemualika staa huyo huku ikinyetishwa kwamba, vigogo wa sanaa hiyo Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ndiyo watakaomsindikiza.
 

“Mapedeshee wamemtumia mamilioni ya fedha Lulu, wanataka kufanya naye pati ya pamoja kwa vile ni miongoni mwa mastaa wa Bongo wanaokubalika nchini humo na pia kumpa pole kwa kukaa gerezani muda mrefu.
 

“Mbali na sherehe hiyo, watakapokuwa nchini humo wanatarajia kuendeleza filamu ambayo wameanza kuirekodi hapa Bongo,” kilisema chanzo hicho.
 

Hata hivyo, chanzo kiliweka wazi kwamba kwa sasa, Lulu si rahisi kusafiri nje ya Bongo kwa vile kesi aliyonayo ina mipaka ya sehemu za kwenda. 
Alipotafutwa Dk. Cheni juu ya ishu hiyo, alisema waliomuita Lulu si mapedeshee bali ni Wabongo waishio kule, lakini masharti ya kesi yake hawezi kusafiri nje ya Tanzania.
Dk. Cheni akaulizwa kuhusu yeye na Steve Nyerere kuwepo kwenye safari hiyo ambapo alisema hana ufafanuzi zaidi, akakata simu.

NAIBU WAZIRI AINGILIA KATI UGOMVI WA LADY JAYDEE NA CLOUDS FM....RUGE AKIMBILIA MAHAKAMANI




IKIWA ni siku moja tu tangu Naibu Waziri wa Habari  Michezo Vijana na Utamaduni Amos Makala kutangaza hadharani kulivalia njuga suala la mzozo kati ya Mkurugenzi wa wa Kampuni ya Clouds Media Group Ruge Mutahaba  na msanii nyota wa kike wa Bongo Fleva Judith ‘Wambura Lady Jaydee’  Ruge ametoa ya moyoni.
Tanzania Daima ambayo ilimpigia simu Ruge na kumuuliza ana lipi la kusema baada ya Makala kutamka kwamba atawaita wawili hao na kuzungumza nao sambamba na kuleta suluhu.
“Mimi kana nilivyosema katika tamko langu wiki iliyopita kwamba niko tayari tuitwe na watu watusikilize  pande zote mbili  hasa mlalamikaji na ukweli uweze kuwa wazi zaidi kwa sababu hadi sasa Lady Jaydee amekuwa akisema mambo mengi kiasi kwamba hata nashindwa kumuelewa”
Na siyo Waziri Makalla tu pia ikiwezekana hata kama kuna watu wengine wanataka kujitokeza ili kutuweka katika kiti moto watuulize maswali na kila mmoja wetu aote majibu mbele ya hao watu mimi niko radhi kufanya hivyo” anasema Ruge.
Wakati huohuo Ruge ameongeza kwamba  tayari ameshafuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfungulia jalada la malalamiko ya kutukanwa na Lady Jaydee na taarifa hiyo amepelekewa  msanii huyo akiitwa katika vyombo vya sheria.
Lakini ninaweza kusema jambo hili linaweza kuzungumzika nje ya vyombo vya sheria kwani sisi tunaliona ni jambo dogo na la mzaha lakini lina athari kubwa katika jamii inayotuzunguka  anasema Ruge.
Mwanzoni mwa mwezi huu Lady Jaydee aliamua kuibuka na kuituhumu Clouds Media Group  kwa kutumia mitandao ya kijamii kama facebook, twitter nab log yake kwamba wana muhujumu kimuziki , kuzuia matangazo ya mgahawa wake wa Nyumbani Lounge   na kipaji chake kwa ujumba tuhuma ambazo Ruge na Clouds wanazikanusha vikali.
Mwandishi wa habari hii alijaribu kumtafuta Lady Jaydee azungumzie kuhusu kauli ya Waziri kwa kupitia simu ya mumewake Gadner Habash simu iliita bila kupokelewa.

JESHI LA TANZANIA LATAMBA TENA.....LINASEMA KAZI YAKE NI MOJA TU AMBAYO NI KUWAFUMUA WAASI WA M23 HUKO KONGO




JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limesema limeanza kuwapeleka askari wake nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC) kulinda amani na kuhakikisha wananyang’anywa silaha zote waasi wa kundi la M23 ili nchi hiyo itawalike.

Kutokana na hatua hiyo, JWTZ limesema halitishwi na vitisho vya M23 kutokana na kujiandaa vizuri kila idara, ikiwa ni lengo la kutaka kuona wananchi wa DRC wanaishi kwa amani, tofauti na sasa ambako kumekuwa na vitendo vya kinyama dhidi ya wanawake na watoto wadogo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, wakati wa kutoa tamko la jeshi hilo, Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, alisema kamwe hawatishwi na kundi la M23.

Alisema wanashangazwa na kitendo M23 kutoa vitisho, wakati askari wanaokwenda huko wanatoka nchi za Afrika Kusini, Malawi na Tanzania.

“Kwa nini iwe Tanzania pekee, sisi hatuwezi kutishwa na kikundi cha wanamgambo 1,000, tunasema tunakwenda kutimiza jukumu la Umoja wa Mataifa (UN) kuhakikisha DRC inatawalika na silaha zote wananyang’anywa,

“Tanzania tuna historia kubwa ya kuleta ukombozi na amani ndani ya nchi za Afrika, zikiwamo Commoro, Afrika Kusini, Liberia, Sudan na Lebanon, ndiyo maana vikosi vyote vitatu vinaongozwa na Mtanzania, Brigedia Jenerali James Mwakibolwa.

“Tulipokwenda Commoro, tulihisi kama damu itamwagika lakini hali ilikuwa tofauti kabisa na isitoshe ni askari mmoja tu aliteleza na kuanguka majini, sasa hawa M23 wao wamepata wapi mafunzo.

“Itakumbukwa Idd Amin Dada, alikuwa anajigamba na kusema anataka kuja kunywa chai Dar es Salaam, lakini aliishia kuchungulia visiwa vya Ukerewe… majigambo ya M23 ni ishara ya kuanza kuwa na wasiwasi,” alisema Kanali Mgawe.

Alisema kikosi kilichoanza kwenda DRC,kinajulikana kama Tanzania Bataria One –DRC (TANZBATT-1 DRC) na kuongeza kwamba kila baada ya miezi sita kutafanyika mabadiliko kadri itakavyohitajika.

Alisema kutokana na vitisho hivyo, bado Tanzania ni salama na itakuwa kuwa salama na kuwataka Watanzania kuondoa hofu juu ya matukio yanayotokea hivi sasa.

Alisema vifaa vya askari, wanaokwenda Kongo vimekamilika na tayari UN imevifanyia ukaguzi na kuridhia vinakidhi mahitaji katika kuimarisha ulinzi na usalama.

Kuhusu mzozo wa Tanzania na Malawi, alisema nchi hizo bado zina uhusiano mzuri wa kidiplomasia.

Mapema wiki hii, Rais Jakaya Kikwete aliwakabidhi askari wa JWTZ bendera mkoani Pwani, ikiwa ni ishara ya kuanza safari ya kuelekea DRC.