Tuesday, July 2, 2013

TAZAMA PICHA:TUZO ZA BILLBOARD AWARDS (BBMA) 2013 ZILIVYOFAANA JIJINI LAS VEGAS...!!



Jana Usiku wa Tarehe 1/7/2013 ulikuwa usiku wa  Tuzo
za Billboard Music Award,Tuzo hizi
ni Maalumu kabisa kwa wanamuziki wanaofanya vizuri na
 nyimbo zao zinazosikilizwa zaidi
kwenye vituo mbalimbali vya redio,television na dunia kwa
kwa ujumla  na Online ni kimaanisha Youtube,Itune na n.k kwa Ujumla......


Usiku wa Jana ndio ilikuwa sherehe ya ugawaji wa tuzo hizo
 uliofanyika kwenye jiji la Las Vegas
uku ikiudhuriwa na Mastaa wengi wanaofanya mziki ndani
 ya marekani na nje ya marekani...
Usiku huo unaweza kujionea kwenye picha jinsi
ulivyofaana kabisa kila mtu akiwa kwenye nyuso za furaha
wakati wa kupokea tuzo na hata wakati wa utumbuizaji

Zifuatazo ni picha za ugawaji tuzo na matukio mbalimbali ya
 utumbuizaji kutoka kwa wasanii
walioalikwa kutumbuiza kwenye usiku huo wa Billboards Award
2013 (BBMA)......



Selena Gomez & Taylor Swift...!!
Akon akitumbuiza kwenye usiku wa Tuzo za Billboard...!!
Nicki Minaj & Lil wayne wakitumbuiza pamoja...!!

Madonna akizungumza kwenye steji kuhusu madawa ya kulevya....!!





Psy & Tracy Morgan wakifanya yao jukwanii...!

Sky Blue akitumbuiza Jukwaa moja na Wiz Khalifa....!!picha zote na dj sek 


Justin Bieber akitumbuiza stejini...!!
Will.Iam akizungumza jukwanii...!!
Msanii mkongwe Prince akitumbuiza jukwanii...!!

Taylor Swift akitumbuiza jukwanii...!!
Taylor Swift akipokea Tuzo usiku wa Tuzo za Billboard...!!
Nicki Minaj akipokea Tuzo...!!
Chris Brown Akitumbuiza...!!

Bruno Mars kwenye Stage....!!
Tracy Morgan ndio aliehendesha Shuguli nzima ya Tuzo hizo..!!


Kelly nae alikuwepo kwenye usiku huo wa Tuzo za Billboard
Madonna & Wil-Iam wakiwa jukwani kuwakilisha Tuzo..!!
Serena Gomez akiwajibika stejini...!!

Taylor Swift akipokea Tuzo...!
Justin Bieber akizungumza baada ya kupokea Tuzo...!!

Pitbull akitumbuiza...!!
Jennifer Lopez akifanya yake stejini.....
Celline Dion akizungumza kwenye usiku wa Tuzo hizo za Billboard kama
mkongwe kwenye muziki wa Marekani...!!
David Guetta akitumbuiza jukwaani pembeni akiwa na
 Akon mkono wa kushoto na kulia kwake ni
Ne-Yo
David Guetta akizungumza baada ya kupokea Tuzo...
Lil wayne a.k.a Tunechi akiwa stejini....
Nicki Minaj & Lil wayne kwenye jukwaa wakitumbuiza kwa pamoja...!!
Ne-Yo akitumbuiza jukwani kwenye usiku wa
 Tuzo hizo za Billboard 2013

HAYA NDO MAMILIONI YA PESA ALIYOINGIZA DIAMOND KWENYE SHOW ZA MWEZI ULIOPITA ....


 

Staa wa Kesho, Diamond ameendelea kupiga hela kwa show nyingi zinazomfuata kila kukicha. Wingi wa show hizi unazidi kumfanya kuwa miongoni mwa wasanii wachache wa Tanzania wenye pesa nyingi zaidi.

Tumejaribu kuangalia baadhi ya show alizofanya mwezi huu, atakazofanya mwishoni mwa mwezi huu na mwezi ujao ili kukadiria ni kiasi gani anaweza kuwa ameingiza. Baadhi ya show tunafahamu ni kiasi gani aliingiza huku zingine tukikadiria kutokana na jinsi anavyochaji.
 
Show ya nchini Comoro 22 June
Katika show hii alisema alilipwa si chini ya dola 25,000 za kimarekani ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 38.
 
Show za Usiku wa wasafi Tabora 28 na 29 June
Mara nyingi katika show za ndani Diamond hachukui si chini ya shilingi milioni 10 kwa show mbili huenda akawa amelipwa zaidi ya shilingi milioni 15.

Show ya Tigo Mwanza 30 June
Katika show za makampuni kama hizi Diamond hulipwa si chini ya shilingi milioni 10.
 
Kili Music Tour 2013
Tulipata taarifa kuwa Diamond atafanya show kwenye mikoa minne na kwamba amelipwa shilingi milioni 50 kwa show zote.
 
Show ya Matumaini 7 July
 kwenye hii show diamond ana zaid ya mil.10

Show ya Kenya 27 July
Kwenye show hii Diamond atashare stage na mastaa wa Nigeria, Ice Prince na Davido na hapa kama alivyosema kuwa katika show za nje ya nchi huwa hachukui chini ya dola 15,000. Kuna uwezekano hapa akawa amelipwa zaidi ya shilingi milioni 20.
 
Kama una calculator basi unaweza ukapiga hesabu mwenyewe ni kiasi gani ameingiza kwa show za June na July. Kumbuka pia kuwa show zote hata za July tayari ameshasaini mkataba na ameshalipwa chake tayari. Kitu kama milioni 140 na usheee!!
 
Pia kumbuka ni balozi wa Cocacola na hulipwa kila mwezi kwa shughuli zinazohusiana na deal hiyo. Katikati wa mwezi July pia kuna uwezekano akawa na show zingine kibao.
 
“Siku zote ishi ukikumbuka, Maisha ni Vita, vita ambayo mwisho wake ni siku ya wewe kuingia kaburini, hivyo haupaswi kuchoka wala kukata tamaa.Heshima, Juhudi na Maombi ndio nguzo pekee zitazokusaidia wewe kushinda Vita hii… tambua Mwenyezi Mungu ndiye Muweza na Mpaganga wa yote,” anasema Diamond.

FEZA KESSY AENDEKEZA TABIA YA KUPIGWA DENDA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER



Mshiriki  wa  Botswana, Oneal   ameendeleea  kuyafaidi  mate  ya  dada  yetu   ambapo  wakati  huu  jamaa  huyo aliamua kupiga magoti wakati akimwaga "sera za nguvu"  kwa Feza na kumwambia kuwa maisha yake yalikuwa shagala bagala kabla hajakutana na mwakilishi huyo wa Tanzania.


Maneno hayo matamu yalimwingia vyema Feza ambaye alikuwa akitabasamu muda wote kuashiria upendo mzito kwa jamaa huyo wa Botswana ambaye anataka wawe na maisha pamoja siku za usoni.


Washiriki wengine waliamka na kuwashangalia wapenzi hao kama yalivyo maisha ya kawaida. 

Muda  mfupi  baadaye, Feza  na  Oneal  walianza  kubadilishana  mate  na  ndimi...!!!!!!! 

http://youtu.be/7XsSMDfimZE

http://youtu.be/7XsSMDfimZE

TAZAMA KWA UMAKINI:: HII NI KUFURU HEBU CHEKI GARI HII AINA YA BUGATTI ILIYOTENGENEZWA KWA DHAHABU.



If you thought flossing and stunting were two unrelated words, one meaning to clean one’s teeth with a string, while the other referring to jumping through a window made of sugar, the English language slang says no!

Flossing and stunting is what “ballers and gangsters” do, and it basically means to show off one's opulent material possessions, and really make sure everybody has seen you, so that you make insecure less financially fortunate people feel uneasy.

Musician Flo Rida can now be added to that category with ease, and while his previous rides were always head turning (and not necessarily in a positive way, may I add), his most recently acquired vehicle beats them all. It’s a gold chrome-wrapped Bugatti Veyron, which stands out, a lot, like you can’t not look at it when it passes by, in all its flossin’ glory.

If you ask me, Flo Rida is a kind of middle-of-the-pack artist in the music industry, and his only way to stand out is not through the quality of his musical works, but the wit with which he can spend his millions. A faux-gold Veyron definitely seems legit, given the current situation, because he is living his "You can have whatever you like" song, which I’ve posted below, for your amusement, and to get the right mood for this piece going nicely. 

The Ride cost a whooping $1.7m.







Wednesday, June 19, 2013

KAHABA APEWA KICHAPO KIKALI BAADA YA KUNASWA AKIJUZA JIRANI NA MSIKITI



Kahaba  mmoja   alijikuta akiambulia kichapo kikali toka kwa vijana wa kiislamu baada ya kunaswa akijiuza karibu na msikiti wao.....
  
Tukio hilo lilishuhudiwa na wanahabari wetu majira ya usiku jirani na msikiti huo uliopo nyuma ya Corner Bar, Kijitonyama jijini Dar ambapo mwanamke huyo na wenzake walikamatwa na baadhi ya vijana waumini wa Kiislamu waliokerwa na kitendo cha wao kutoa huduma haramu ya ngono maeneo hayo.


Baada ya wenzake kufanikiwa kutoka nduki mwanamke huyo alishuhudiwa akila bakora kisha akapelekwa katika Kituo cha Polisi Kijitonyama, Dar akaunganishwa na wengine waliokamatwa usiku huo.

Ilielezwa kuwa wanawake hao wamekuwa wakiuza miili kwa wanaume karibu na msikiti huo na pembezoni mwa baa hiyo.

Ilisemekana kuwa kumekuwa na kawaida ya wanawake hao kusimama maeneo ya nyumba hiyo ya ibada na kufanya biashara hiyohuku wakichafua mazingira kwa kutupa ovyo kondomu na kujisaidia maeneo hayo.
 Wakati mwanamke huyo akicharazwa bakora, nguo ya ndani ilimvuka huku akipiga kelele kuwa hatarudia kufanya hivyo na kama akirudia basi akatwe kichwa.

Kutokana na kukerwa na vitendo hivyo, vijana hao wanaofanya ibada katika msikiti huo, waliamua  kuwatafuta vijana wa ulinzi shirikishi na kuwapa kazi hiyo ya kuwakamata na kuwacharaza bakora kisha kuwapeleka katika kituo hicho cha polisi.
 

“Tumeamua kuwakamata na kuwacharaza bakora, hawana ustaarabu wala busara hawa, wanakojoa na kutupa kondomu  hovyo, “ alisikika mmoja wa vijana hao.
  
Mmoja wa vijana hao aliyekuwa akisimamia kwa karibu zoezi hilo, aliwaambia waandishi wetu kuwa wameamua kufanya hivyo na litakuwa zoezi endelevu kutokana na wanawake hao kutokuwa wasikivu kwani kila wanapoambiwa juu ya kukaa mbali na nyumba hiyo ya ibada hawasikii.

Alisema kuwa siku moja wanawake hao walimtoa udhu muumini mmoja ambaye alikuwa akienda kuswali alfajiri baada ya kumshika na kusababisha akose kuhudhuria swala siku hiyo.



Hata hivyo, wakati mahojiano yanaendelea, mmoja wa askari waliokuwa zamu aliamuru mwanamke huyo aingizwe lokapu kusubiri kesho yake aunganishwe na wenzake kisha wapelekwe mahakamani.

Habari zilizotufikia  ni kwamba baada ya kufikishwa mahakamani na kukutwa na kosa la uzururaji, wakahukumiwa kifungo cha miezi sita jela au faini ya shilingi elfu hamsini ambapo walilipa kiasi hicho na bado wanaendelea na biashara hiyo maeneo hayo.

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKOA WA ARUSHA



Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetuma salamu za rambi mbali kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Muhongo kutokana na vifo vya wananchi watatu wa Mkoa huo vilivyotokea kufuatia mripuko wa bomu uliotokea juzi katika viwanja vya Soweto Jijini Arusha.

Watu wasiopungua 70 waliripotiwa kujeruhiwa wakati wa mripuko huo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi katika Kata ya Soweto wa Chama cha Demokrasia ya Maendeleo { Chadema }.

Katika Taarifa ya rambi rambi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyotumwa kwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha na kutiwa saini na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alielezea kupokea kwa masikitiko na huzuni taarifa ya shambulio la kigaidi la bomu lililotokea tarehe 15 Juni mwaka 2013.

Balozi Seif alisema Taifa kwa mara nyengine tena limekumbwa na msiba wa njama za kigaidi zilizoua na kujeruhi rMkuu wa Koa wa Arusha aia wema wasio na hatia sambamba na tukio jengine linalofanana na hilo lililogharimu roho za wananchi wengine wakati wakiwa katika ibada Kanisani.

Balozi Seif alisema kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wananchi na yeye binafsi anatuma salamu hizo za rambi rambi kutokana na maafa hayo na kuwaombea marehemu malazi pema na majeruhi wapone haraka ili waungane na wenzao katika ujenzi wa Taifa.


Halkadhalika Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaiunga mkono Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada zake za kupambana na ugaidi wa aina yoyote hapa Nchini.

Alieleza kwamba SMZ na Wananchi wa Zanzibar wako pamoja na wenzao katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na maombolezo na kuwaomba wafiwa wawe na moyo wa ustahamilivu, uvumilivu na subra katika kipindi hichi.

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kutenga shilingi Milioni Mia Moja { 100,000,000/-} kama zawadi kwa kwa mtu ye yote atakayetoa Taarifa zitakazofanikisha kunaswa kwa mhalifu au watu wenye mtandao wa ulipuaji wa mabomu hapa Nchini.

Saturday, June 15, 2013

DIAMOND AMSUTA MGANGA WAKE..!!!


STAA anayeng’aa katika Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemsuta mganga aliyejitokeza na kudai kwamba mwaka huu staa huyo hatapata mafanikio yoyote na atapotea katika fani. 

Mganga huyo ambaye alidai utaalamu wake ndiyo uliompandisha chati Diamond alisema mwaka huu staa huyo hatapata tuzo, atafifia na jina lake litasahaulika kutokana na kukiuka masharti yake.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Diamond alisisitiza kutomtambua mganga huyo na anamshangaa kwa kuwa mwaka huu amepata mafanikio tofauti na alivyosema.

“Hebu angalieni, mganga alidai mwaka huu nitafutika katika fani, mbona nimepata tuzo mbili kwenye Kil na nimechaguliwa kuwa balozi wa Cocacola na shoo zinajaza kinoma?” alihoji Diamond
.
Aidha, alisema shoo zake bado zinajaza watu wengi huku akiitolea mfano ya mwisho iliyofanyika Dar Live, Mbagala Zakhem, Dar hivi karibuni iliyojaza nyomi ya watu.

BABA AMKANA MTOTO KISA ANA NYWELE ZA KIARABU.....MAMA AKASIRIKA NA KUMTUPA, POLISI WAMTIA MBARONI



Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Khadija Idd anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro  akidaiwa kumtupa barabarani mtoto wake mwenye umri wa miezi 6 baada ya mwanaume aliyezaa naye kumkataa. 

Shuhuda wetu ambaye ni dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Shabani, alisema tukio hilo lilitokea Juni 11, mwaka huu maeneo ya Mafiga karibu na Msikiti wa Mahita ambapo Khadija alichukua uamuzi huo baada ya mwanaume aliyezaa naye kumgomea mtoto kwa madai ana nywele za Kiarabu hivyo si wake.


“Huyu dada alifika kwenye kijiwe chetu akiwa amembeba mtoto mgongoni na kukodi pikipiki ili nimpeleke mjini.
 
“Tulipofika kwenye msitu uliopo karibu na mashamba ya SUA, aliniambia niendeshe spidi kuna mtu anamuwahi. 

Nilitii amri lakini tulipofika mbele kidogo nikashangaa anamtupa yule mtoto.


“Nilipoona vile nilisimama na kumhoji kwa nini anafanya vile, akawa hajibu. Nikamchukua na kumpeleka kituo kikuu cha polisi akiwa hana mtoto. Baadae wasamaria wema walimuokota mtoto akiwa ameumia na kumfikisha polisi,” alisema mtoa habari huyo.


 


Mwandishi wetu alifika katika kituo hicho cha polisi na kufanikiwa kumkuta Khadija akiwa chini ya ulinzi mkali huku mwanaye akitokwa na damu usoni na alipoulizwa kulikoni alisema:
 
“Jamani naomba msamaha, nimefanya hivyo kwa hasira baada ya baba wa mtoto kudai si wake, eti ni Mwarabu wakati yeye ni Mngoni wa Songea, nisameheni sitarudia tena.”


Akizungumza na mwandishi wetu, Kaimu Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Morogoro, Tausi Mbalamwezi alisema mwanamke huyo amefanya kitendo kibaya na sasa wanamsaka baba wa mtoto ili amlee huku mtuhumiwa akisuburi taratibu nyingine.

 “Yupo hapa na tumemkuta na kadi ya kliniki ikionesha kuwa, baba wa mtoto anaitwa Costa Haule. Huyu hana nia njema na mtoto kwani alitaka kumuua kwa hiyo baada ya kumtibia tunawatafuta ndugu wa mwanaume au baba wa mtoto ili wamlee wakati tukiandaa utaratibu wa kumfikisha mahakamani,” alisema Afande Tausi.