Thursday, April 25, 2013

"WANAUME NI TAPELI NA WAMENIPOTEZEA MUDA WANGU"...QUEEN SUZY




MNENGUAJI wa Bendi ya FM Academia, Suzan Chubwa ‘Queen Suzy’ amesema hahitaji mwanaume yoyote kwa sasa kwani wanampotezea muda kwa kipindi kirefu.

Akizungumza na mwandishi wetu,Queen alisema wanaume wamekuwa wakimsumbua mara kwa mara kutaka kampani ya kimapenzi lakini wengi wao wanakuwa hawana mapenzi ya kweli hivyo anaona bora kuwapiga chini.

“Bora niwe singo natafuta pesa kuwazawaza hawa wanaume nitaishia kuumia tu na kushindwa kufanya shughuli zang, tena waache kunifuatafuata kwa sasa,’’alisema Queen Suzy.


Mnenguaji huyo alishawahi kuwa na uhusiano na mwimbaji wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Kalala Junior ambaye alizaa naye mtoto mmoja baadaye akatembea na rapa wa FM Academia, G 7 ambao wote ameshamwagana nao. 

No comments:

Post a Comment