Monday, May 27, 2013

RIHANNA IMEKULA KWAKE..!!!!! ...KARRUECHE TRANS SASA AHAMIMIA NYUMBANI KWA CHRIS BROWN




Siku zote mwenye kiu iliyopitiliza akipewa maji ya kunywa hutamani atumie jagi zaidi ya kikombe anachowekewa maji, ndivyo ilivyomtokea mrembo Karrueche Tran aliyetoswa mwaka jana na Chris Brown aliyemchagua Rihanna dhidi yake wakati mrembo huyo akiwa na moyo uliojaa mapenzi na maumivu ya kulikosa penzi la ‘turn up the music singer’..
Sasa alipopewa nafasi tena ameamua kuitumia vyema na katika kupunguza zaidi umbali ameamua kuhamia kabisa nyumbani kwa mwimbaji huyo. 


Kwa mujibu wa TMZ Chris na Karrueche wamekua wakiishi pamoja nyumbani kwa muimbaji huyo Los Angeles tangu walipoonekana pamoja kwenye sherehe ya kuzaliwa Chris Brown alipotimiza miaka 24. 
Ripoti zinasema mrembo huyo amehamishia nguo zake na vitu vyake takribani vyote kutoka kwake na kuvipeleka nyumbani kwa Chris Brown lengo ni kuwa karibu zaidi na mwimbaji huyo. 

Rafiki wa karibu wa KT ameuambia mtandao wa Hollywoodlife kuwa karrueche anajaribu kuweka commitment katika mahusiano yake na Chris ambayo mwimbaji huyo hawezi kuitunza lakini ameamua kujiweka kwenye mstari huo kwa ajili ya mahusiano yao. 

Chanzo hicho kiliongeza kuwa Karrueche anampenda Chris kwa sababu wanaendana na anapenda upande mwema wa Chris Brown. 

Inawezekana Karrueche hamhofii tena Rihanna kwa kuwa mwaka jana alilazimika kuisomba mizigo yake kutoka kwenye nyumba ya mwimbaji huyo baada ya kumwagwa na himaya yake kuchukuliwa na RiRi bila sababu za msingi isipokuwa Chris kuamua tu kumrudisha RiRi. 


Kwa sasa Chris na Rihanna hawako pamoja tena na Karrueche anaonekana kukaba nafasi yake vizuri. Swali, je hii pembe tatu ya mapenzi yaliyojaa drama itaishia hapo au baadae itambidi KT aondoe tena mizigo yake kumpisha Rihanna?

No comments:

Post a Comment