Sunday, June 2, 2013

HUDDAH TOKA KENYA AYAAGA MASHINDANO YA BIG BROTHER..... MWAKILISHI WA TANZANIA ALIA NA WAVUTA BANGI


Maneno  huumba....!!!  Huddah  ameliaga  shindano hilo...
------------------------
Huddah ambaye ni mshiriki kutoka Kenya   alijikuta akibubujikwa na machozi  jana wakati akimuelezea Angelo (SA) kuhusiana na uhusiano wake wa kimapenzi ambao ni wa ku-beep yani vuta nikuvute ambao amekuwa nao nchini kwao.

Mrembo huyo hakutaja jina la mpenzi wake lakini inahisiwa alimaanisha kuwa katika mahusiano na Rapper Prezzo wa Kenya. Kwa muda sasa kumekuwa na umbea mtaani kuhusiana na uhusiano wa kimapenzi kati ya wawili hao lakini haijafahamika kinaga ubaga kama Huddah alimaanisha kum-miss Mr. President. ..

Mrembo huyo akizidi kufunguka, alielezea jinsia anavyo-miss mabusu motomoto, anavyo-miss kung'atwa shingoni n.k. “I miss the way that he kisses me. I miss him biting my neck”.. 
LEO  MACHOZI  YAKE  YAMELIPWA  BAADA  YA  MREMBO HUYO  KUONDOLEWA  NDANI YA  JUMBA  HILO....Mashabiki  wamepiga  kura  ya  kumwondoa  ili  asiendelee  kumlilia  mpenzi wake.....
Mshiriki mwingine  aliyeaga  mashindano  hayo  ni  Denzel wa Uganda....

KWA UPANDE MWINGINE, mrembo wa Tanzania ,Feza anayeiwakilisha Tanzania alijikuta katika simanzi kali wakati alipoelezea kuhusu jinsi ambavyo kaka yake aliteseka kutokana na kujihusisha na madawa ya  kulevya .. 'drugs'.
Feza alitumia fursa hiyo kuwasihi watu hasa vijana kujiepusha kabisa na madawa ya kulevya kwani ni hatari sana katika jamii inayotuzunguka..

No comments:

Post a Comment