Tuesday, April 9, 2013

LAANA: MWALIMU MKUU AMTIA MIMBA MWANAFUNZI NA KUMLAZIMISHA AITOE



 Polisi wa  Kituo  cha Nandi  chini Kenya wanamshikiria  mwalimu  mkuu  wa  shule  ya  msingi  St. Paul  kwa  kosa  la  kumpa  mimba  mwanafunzi  wa  darasa  la  sita  na  kisha  kumlazimisha  aitoe....

Kwa  mujibu wa bodi  ya  shule  hiyo, mwalimu  huyo  amekuwa  akifanya  mapenzi  na  mwanafunzi  huyo  wakati  wenzie  wakijisomea  darasani nyakati  za  usiku  katika  masomo  ya  jioni.....

Binti  huyo  aliyekumbwa  na  mkasa  wa  aibu alikuwa  ni  kiranja  mkuu  wa  shule  hiyo  na  inadaiwa  kuwa  mwalimu  mkuu  ndiye  aliyesimamia  uteuzi  wa  binti  huyo  ili  aweze  kumnasa  kiulani.....
Habari  zinadai  kuwa baada  ya    mwalimu  huyo  kugundua  kuwa  binti  huyo anamimba, mipango  ya  kuitoa  mimba  hiyo  ilianza  mara  moja....

Kwa mujibu  wa  mwalimu  mmoja  wa  shule  hiyo,Zoezi  hilo  chafu  lilifanyika  katika  hospitali  ya  wilaya  ya  Kapsabet  na  kwamba  wakati  oparesheni  hiyo  haramu  ikifanyika, walimu  wenzake  walipata  taarifa  kutoka  kwa  mmoja  wa  manesi  wa  hospitali  hiyo  na  ndipo  walipochukua  hatua  ya  kuwajulisha  wazazi  wa  binti  huyo  ambao  waliamua  kwenda  polisi..... 

No comments:

Post a Comment